Na Yusuph Mussa, Korogwe
KATIBU Mkuu
wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Bw. Nicholaus Mgaya,
amewataka wafanyakazi wote nchini kuungana na shirikisho hilo ili kutoka na msimamo
wa kumchagua rais wa awamu ya tano mwaka 2015.
Alisema muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini Afrika Kusini,
siku zote ndio unaochagua rais wa nchi hiyo; hivyo kama wafanyakazi wote
wataungana na TUCTA, wataweza kuchagua rais wamtakaye ili matatizo yao yaweze
kutatuliwa.
Bw. Mgaya aliyasema hayojana katika warsha ya siku
nne inayofanyika mjini Korogwe, mkoani Tanga ambapo unahusisha wawakilishi wa
wafanyakazi katika wilaya zote mkoani humo.
"Kabla ya
kupiga kura, wagombea wote wa nafasi ya urais tutawaita na kuwapa masharti juu
ya kiongozi tumtakaye, nguvu ya chama ni wanachama ambao tukiwa wengi, tuna
uwezo wa kumchagua rais ajaye kama ilivyo Afrika ya Kusini," alisema.
Aliongeza kuwa, kwa sasa kuna utitiri wa
vyama vya wafanyakazi, vingine vikiwa kwenye mikoba hivyo kama wanataka
kupambana na Serikali ili kutetea masilahi yao lazima waungane.
"Kwa sasa tuna vyama 30 vya
wafanyakazi, bado kuna vingine vipo kwenye mikoba...ni vyema msajili wa vyama
akaliangalia hili maana chama kina miaka mitano, lakini hakina usajili.
"Wafanyakazi wanapinga Rasimu ya Katiba Mpya
na kusema haijaweka vitu vingi vinavyowahusu wafanyakazi kama mgomo, lakini kwa
vile tumepewa fursa ya kuijadili rasimu husika basi wafanyakazi wote wahudhurie
mikutano ili kuipinga," alisema.
Bw. Mgaya alisema ikiwezekana wafanyakazi wafanye hata maandamano kama
katiba hiyo haitaingiza mgomo badala yake limeingizwa suala la Serikali tatu.
Alisema mgomo ni haki ya wafanyakazi
ambapo nchi tatu pekee barani Afrika ambazo katiba zao ndizo zimeruhusu mgomo
nazo ni Kenya, Ghana pamoja na Afrika Kusini.
Awali, Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka
(TUCTA), Makao
Makuu, Bi. Margareth Mandago alisema wafanyakazi
hawawezi kutetea haki zao kama hawazijui hivyo wamedhamiria kutoa mafunzo nchi
nzima ili wanapopigania masilahi yao waweze kutambua kanuni, sheria na taratibu
za kupata haki hizo
No comments:
Post a Comment