25 July 2013

TUNAHITAJI MIAKA 240 KUUAGA UMASKINI - DKT.GABAGAMBI



 MHAD HIRI w aCh uoKikuuchaKilimoc haSo koine (SUA), Dkt . DamianGabagambi,amesema ina hitajimi aka240kua nziasasailikuwe zakuto kom ezauma skini uliokithirikwawananchinchini,anaripoti Mw anadishi Wetu, Morogoro.


Ha yoyalibainishwamji ni hapajanana Dkt. Gabagam bi,wakati wamkut anom kuuwaMtandaowa Vik undivya Wak ulim a Tanza nia(MVIWATA).Alisema hali hiyo inachangiwa na kiwango kidogo cha kupunguza umaskini nchini tangu mwaka 1992 hadi mwaka 2011. “Tangu mwaka 1997 hadi mwaka 2011 umasikini umepungua kwa asilimia 2.1, hivyo kwa mtindo huu tukitaka kupunguza umaskini hadi asilimia 10, tutahitaji miaka 169 na kuutokomeza kabisa ni inahitaji miaka 240,” alisema.

Alisema ili nchi iondokane na hali hiyo, ni lazima kuwapo na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika sekta husika. A l i s e m a w a k u l i m a hawashirikishwi katika kuandaa mipango ya kupambana na , hivyo kusababisha changamoto zilizopo kwenye kilimo kuendelea kubaki zile zile pamoja na kuwapo kwa juhudi mbalimbali.

Dkt.Gabagambi, aliishauri Serikali kubadili mtindo wa ushirikishaji wa wadau ubadilishwe ili washirikishe wengi zaidi, kwani kushirikisha watu wachache ni ulaghai.Naye Profesa Amon Mattee, kutoka SUA aliwashauri wakulima na wafugaji kuzingatia sera katika masuala yote yanayohusu kilimo pamoja na kujitambua katika kukuza maslahi yao katika mchakato wa sera.

“Wakulima na wafugaji kutokuwa na ajenda na kutegemea viongozi wa serikali au kuwasema ni tatizo, kukosa sauti na msukumo wa pamoja katika mambo yanayowahusu ni tatizo, hivyo mnapaswa kuondokana na dhana hizi ili kulima kilimo chenye tija,” alisema.

Aliwataka wakulima watambue kuwa, wana haki na wajibu katika mchakato wa kuandaa sera pamoja na kuainisha mambo yanayowagusa, kwani wao ni kundi maalum ambalo lina tija kwa maslahi ya taifa.

No comments:

Post a Comment