RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,
Dkt. Ali Mohamed Shein kesho anatarajia kufungua maonesho ya wakulima Nanenane
mkoani Dodoma na kufungwa na Rais Jakaya Kikwete, anaripoti Mariam Mziwanda.Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika mhandisi
Christopher Chiza alisema kuwa Sikukuu ya Wakulima Nanenane mwaka huu
inatarajia kufanyika tena Kitaifa mkoani Dodoma katika Viwanja vya Nzuguni,
Manispaa ya Dodoma.
Alisema sherehe
hizo ambazo kwa kiasi kikubwa hujikita zaidi katika kuonesha mafanikio na
changamoto za sekta ya kilimo zitahusisha wadau wote kuanzia ngazi ya kijiji
hadi Taifa lakini badala ya kumalizika Agosti 8, mwaka huu kama ilivyozoeleka
zitahitimishwa mnamo Agosti saba kutokana na kuingiliana na sikukuu ya Idi El
Fitri.
Alisema
sherehe hizo zinaandaliwa na kuratibiwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya
Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na Chama cha Wakulima Tanzania (TASO) huku
washiriki wakubwa wakiwa ni wadau wa sekta ya Kilimo, mifugo, uvuvi, ushirika,
wajasiriamali, wizara, taasisi za serikali, sekta binafsi na watoa huduma
wengine na kaulimbiu ya Nanenane mwaka huu ni 'Zalisha Mazao ya Kilimo na
Mifugo kwa Kulenga Mahitaji ya Soko'
No comments:
Post a Comment