29 July 2013

SSRA NA MKAKATI WA KUWAINUA WALIMU



Na Darlin Said
SEKTA ya elimu ni miongoni mwa sekta muhimu katika kuhakikisha Serikali inafikia malengo yake ya milenia ya kukuza uchumi na kuleta maendeleo hapa nchini.Kuthibitisha hilo, kuna msemo unaosema kuwa elimu ndio ufunguo wa maisha, msemo huo ukiwa na maana ya kuwa bila ya elimu hakuna maendelo.
Elimu ikipewa kipaumbele itasaidia kuwepo kwa wataalamu katika sekta mbalimbali hali itakayosaidia kupiga hatua kimaendeleo na kuondoa umaskini katika jamii
.Kwa kulitambua hilo Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii (SSRA) mbali na majukumu yake, imekuwa mstari wa mbale kuhakikisha walimu wanajiunga na hifadhi ya jamii ili kufikia malengo yao pamoja na kuwa salama katika sehemu zao za kazi ili waweze kutoa elimu iliyo bora.Hivi karibuni SSRA ilifanya kongamano liliowahusisha Chama cha Walimu Tanzania (CWT), ambalo lilifanyika mkoani Morogoro.
Katika kongamano hilo Afisa Mwandamizi wa SSRA, Bw.Frank Kilimba anasema chama hicho cha walimu CWT kina jukumu la kuwakilisha maslahi ya wanachama wake katika Sekta ya Hifadhi ya Jamii.Pia Bw.Kilimba anasema CWT lazima ihakikishe inatoa elimu na uhamasishaji kuhusu Hifadhi ya Jamii miongoni mwa wanachama wake ambao ni walimu.
“CWT kwa kufanya hivyo itawasaidia walimu walio wengi hasa waliopo vijijini kujiunga na mifuko hiyo ili waweze kujikomboa hasa baada ya kustaafu,”anasema Bw.Kilimba.Mbali na walimu Bw. Kilimba anatumia nafasi hiyo kuelezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo katika uhamasishaji wa shughuli mbalimbali kwa lengo la kuongeza wigo wa hifadhi ya jamii kwa watu wote.
“Hivi sasa kila Mtanzania aliye katika ajira binafsi au anayejiajiri anaweza kuamua kujiunga na kuchangia Mfuko wa Msingi wa Hifadhi ya Jamii anaoupenda.
Anasema kwa mujibu wa takwimu za SSRA mwaka 2011 takribani watu milioni 1.5 ndio waliokuwa katika huduma za hifadhi ya jamii na hadi kufikia mwaka 2012 pamekua na watu milioni 1.7 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 13.Hivyo SSRA inafanya kazi bega kwa bega na vyama hivyo vyenye kusimamia maslahi ya wafanyakazi hasa katika masuala ya hifadhi ya jamii ili kumsaidia mfanyakazi pamoja na kuleta maendeleo hapa nchini.
A l i o n g e z e a k w a kusema waajiriwa au wanaojiajiri wanayo haki ya kujiunga na mifuko ya hiari wanayoipenda ili waweze kujiwekea akiba itakayowasaidia pale watakapohitaji hasa baada ya kustaafu.
Mbali na hilo anasema mfuko unatakiwa kutoa namba maalumu na kadi ya uanachama kwa kila mwanachama wa mfuko husika.
Wakati huo huo, Bw.Kilimba anasema kuwa kwa hivi sasa ni haruhusiwi mwajiri yeyote kumchagulia mwajiri wake mfuko wa hifadhi ya jamii tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma.Bw.Kilimba anaongezea kwa kusema vilevile mfuko mmoja haupaswi kumwandikisha kwa mara ya pili mwanachama ambaye tayari ameandikishwa na mfuko mwingine wa msingi.
“Muongozo huu auhusu Mfuko wa Bima ya Taifa (NHIF) na Mifuko ya Hiari (Supplementary Scheme),” Bw. Kilimba aliongezea kwa kusema.Mbali na hilo anatoa wito kwa waajiri kujitahidi kutoa fursa sawa kwa mifuko yote ya hifadhi ya jamii kuweza kutoa elimu ya mipango ya mafao kwa wanachama, kwa namna yoyote mwajiri asitoe tamko wala mwelekeo wa kumtaka mwajiriwa kuwa mwanachama wa mfuko fulani.
Anasema kufanya hivyo ni kumnyima mfanyakazi haki ya uhuru wa uchaguzi wa mfuko anaoupenda mwajiriwa.Aidha nasema mifuko ya hifadhi ya jamii ina wajibu wa kutoa elimu kuhusu haki, wajibu, taratibu za kujiunga na kupata mafao.
Awali Bw. Kilimba anasema mfuko wa hifadhi ya jamii kwa hivi sasa hauruhusu mwanachama yeyote kuhama kutoka mfuko mmoja kwenda mwingine.Anasema mwanachama mtarajiwa anaweza kuchagua mfuko wa kujiunga, pia na yule anayekaribia kustaafu anaweza kuunganisha vipindi vyake vya uchangiaji kutokana na mabadiliko ya ajira yake alijikuta amechangia mfuko zaidi ya mmoja.
SSRA inaendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Hifadhi ya Jamii ili kuleta ustawi na maendeleo kwa wananchi.
Anasema jitihada hizo ni pamoja na mamlaka kurejea kanuni na sheria mbalimbali, tathmini za mifuko ya hifadhi ya jamii, kurejea vikokoto vya mafao, mifuko kufanya mikutano ya mwaka kwa kuwahusisha wadau mbalimbali pamoja na jitihada nyinginezo nyingi zinazoendelea kuboresha sekta hii.
Pia anasema SSRA ipo katika mchakato wa kufanya mabadiliko ambayo yatamuezesha

No comments:

Post a Comment