- AHAMASISHA MAANDAMANO KUPINGA VIONGOZI MAFISADI
- HARAMBEE ZA MAMILIONI YA FEDHA KILA WIKI ZAMTISHA
Na
Waandishi Wetu
WA Z I R I w a A f r i k a Mashariki,
Samuel Sitta, ameunga mkono Tanzania
kuwa na mfumo wa Serikali tatu lakini sio marais watatu na kwamba wanaopigania
jambo hilo
wanataka kugombania madaraka.Sitta
alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana wakati wa ufunguzi wa majadiliano ya
Rasimu ya Katiba Mpya lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Vijana la Katiba
nchini.
Alisema
mfumo wa kuwa na marais watatu utaongeza gharama, hivyo ni vyema ziwepo
Serikali tatu ambazo zitaongozwa na rais mmoja. Alisema fedha ambazo
zingetumika kuhudumia Serikali yenye marais watatu zitatumika kwenye sekta za
afya, elimu na kilimo."Leo
tukiwa na marais watatu, mmoja aende China, mwingine Uingereza sijui
wapi sasa hizo gharama zitatoka wapi?"Alihoji.
Ubinafsi wa
viongozi
Katika
hatua nyingine, Waziri Sitta amewataka Watanzania kuandamana kupinga viongozi
walafi na wabinafsi wanaotaka kujilimbikizia mali.Alisema
kwa hata Tanzania
iwe na Katiba nzuri namna gani bila wananchi kupigania maadili ikiwa ni pamoja
na kuandamana kupinga viongozi wa aina hiyo.
"Katika
nchi yetu tumekuwa na viongozi wengi wa kijamii ambao ni walafi sana na wabinafsi, kama
vijana hamtakuwa mstari wa mbele kuwapinga basi nchi yetu
haitatawalika,"alisema, Sitta.Akifafanua
zaidi alisema haiwezekani baadhi ya watu wachache wawe matajiri wakubwa huku
wananchi wengi wakiwa masikini kupitiliza. "Kama
ni suala la akili watu wote wanazo akili, inakuwaje wao tu ndio wawe
matajiri?" Alihoji.
Alisema ni vema
katiba mpya ielekeze utungaji wa sheria zitakazozuia ubinafsi, udikteta,
ubaguzi, ikiwa ni pamoja na kuzuia kiongozi kufanya kazi kwa masilahi yake
binafsi.Alifafanua zaidi
akisema ili nchi ipate maendeleo, Serikali inatakiwa kupunguza fedha katika
utawala na kuzielekeza katika miradi ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu.
Alisema kuna baadhi
ya viongozi (bila kuwataja) wameanzisha kampuni hewa kwa lengo la kujipatia
fedha, lakini uchunguzi unafanyika dhidi yao
bila matokeo kutangazwa.Alihoji uchunguzi wa
aina hiyo utafanyika hadi lini? "Kumebainika kuwa kuna kampuni tatu hewa
ambazo zinajipatia fedha kwa njia isiyo halali, uchunguzi unafanyika ili
kutafuta ukweli, japokuwa hatuambiwi matokeo ya uchunguzi mara baada ya
kukamilika, nchi yetu itaendelea kuwa ya uchunguzi hadi lini?"Alihoji
Bw.Sitta.
Katika hatua nyingine,
Sitta amewashangaa baadhi ya viongozi nchini wanaohifadhi fedha zao nchi za nje
na kuhoji lengo lao ni nini?Alisema siku hizi
vyombo vya habari vinafanya kazi nzuri ya kuwafichua viongozi wabadhirifu h i v
y o k u s a i d i a wa n a n c h i kuwafahamu.
Harambee
makanisa
Waziri Sitta
alipoulizwa na waandishi wa habari maoni yake kuhusiana na watu wanaotoa
misaada makanisani, alijibu kuwa hata yeye kipindi cha nyuma aliwahi kusimamia
kujenga msikiti wilayani Mirambo, lakini haikuwa shida.
"Lakini kwa sasa
viwango vinatisha mtu anachangisha mamilioni ya fedha kila wiki...hii
inatisha," alisema na kuhoji kuwa watu hao fedha wanazipata wapi? Alisema
kuwa inawezekana nyuma yao
kuna watu wanaowasaidia.
Mrema anena
Kwa upande wake
Mbunge wa Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, Augustino Mrema, alisema mfumo wa
Serikali tatu gharama kubwa kiuendeshaji na utasababisha migogoro nchini.Akizungumza na Majira,
Mrema alisema kuwa Serikali tatu zinafaa kinadharia na sio kiutekelezaji
kwani zitaweza kuhitaji gharama kubwa katika uendeshwaji wake.
“Maoni yangu binafsi
juu ya rasimu mpya ya uundwaji wa Katiba Mpya, kuwa Serikali tatu inafaa
kinadharia na sio kiutekelezaji, mfano kuwepo kwa Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Tanzania na Serikali ya Zanzibar nani atagharamia hizo
Serikali?" Alihoji.
Aliendelea kuhoji;
" Huku kuwe na mabunge matatu na la muungano, pia kuwe na Ikulu ya
muungano, Ikulu ya Tanzania
na Zanzibar,
nani atakayeweza kugharamia Serikali zote tatu‚“ alihoji Mrema.
Imeandikwa
na Kassim Mahege, Frank Monyo Penina Malundo na Neema Malley
Serikali tatu ndio suluhisho la matatizo ya muungano na haiepukiki,kama tatizo ni maraisi watatu basi serikali ya zanzibar na ile ya Tanganyika zipewe uhuru wakutoa jina wanalotaka kumwita kiongozi wa serikali zao,Sisi Znz tutatumia Raisi na Tanganyika wataamua wenyewe,wkimwita gavana,au W mkuu,au chifu sawa tuu.suala la gharama halina msingi wowote kwani sasa hivi Rais wa zanzibar anahudumiwa nanani? Tanganyika itabeba gharama zake zenyewe kama ambavyo zanzibar inabeba gharama zake,watanganyika mnawasiwas wanini na mnarasilimali kibao.
ReplyDeleteSerikali tatu hapana, ni gharama kubwa.Labda kulinda Muungano kwa gharama yoyote.
ReplyDeleteSerikali Tatu serikali mbili vyote ni ushenzi tu kama kweli tunajivunia mshikamano basi serikali ya zanziba ivunjwe tuwe na serikali moja tu ya muungano wa Tz.
ReplyDelete