Na Mwandishi wetu
UJENZI wa majengo marefu jijini Dar es
Salaam unazidi kuleta hofu baada ya kubainika jengo la ghorofa zaidi ya saba
lenye nyufa kiasi cha kutishia maisha ya wanaolitumia na wapitanjia.Uchunguzi
uliofanywa na Majira umebaini kuwa jengo hilo
lipo mtaa wa Asia na Mali
karibu na kituo cha mafuta Barabara ya Samora jijini Dar es Salaam. Jengo hilo lina nyufa nyingi
kiasi cha kutishia wapita njia na baadhi ya watumiaji wake.
Mmiliki
wa jengo hilo alipotakiwa kutolea ufafanuzi hali hiyo na sababu ya kuruhusu
liendelee kutumika alijibu kuwa; "Kama unataka kuandika habari kuhusu ufa
kuna majengo zaidi ya 10 ambayo yana nyufa hapa Dar es Salaam kama upo tayari
nikupeleke ili nikuoneshe hayo majengo na ukitaka kuandika uanze na hayo,"
alisema.
Alisema
kila baada ya siku wakaguzi kutoka manispaa ya Ilala hufika katika jengo hilo kulikagua, hivyo
majibu yote yanapatikana manispaa hiyo."Mimi
sina jibu la kukwambia zaidi ya wewe uende manispaa ndio watakupa majibu yote
unayotaka... sawa?"Alisema mmiliki wa jengo hilo.
Kwa
upande wake mwakilishi wa kampuni iliyojenga jengo hilo (jina tunalo) alisema
jengo hilo lilianza kujengwa mwaka 2006 na kukamilika 2008 hivyo lina miaka
zaidi ya sita sasa.Alisema
kama lingekuwa na matatizo basi wasingepewa vibali vya kuruhusu kutumika.
Alisema tangu lilipoanza kujengwa lilikuwa linakaguliwa na mamlaka husika hadi
lilipomalizika kujengwa, kwani lina vibali vyote na ndio maana watu
wanalitumia.
"Ukitaka kufuatilia basi lazima uende kwenye mamlaka husika utapata hicho
unachokitafuta," alisema ofisa huyo. Baadhi ya
wapangaji katika jengo hilo walisema wao wamekuwa wakimuona mmiliki wa jengo
hilo na mhandisi wa kampuni iliyolijenga wakifika katika jengo hilo mara kwa
mara na kulikagua, lakini hawaelewi ni kwa nini wanafanya hivyo.
"Huwa
tunawaona mmiliki wa jengo hili na injinia ambaye amelijenga jengo hilo mara
kwa mara wanakuja mbele ya jengo na kisha kuelekezana kuelekea juu kwa kuwa
hatuelewi basi huwa tunawaangalia tu, lakini kumbe kuna ufa sasa ndio tumejua
ni kwa nini wanafanya hivyo," alisema mmoja wa wapangaji na kuongeza kuwa
kipindi cha milipuko ya mabomu katika kambi ya Jeshi Mbagala, jengo hili lilitikisika
sana hadi wakaamriwa wafunge maduka watoke.Juhudi za kumtafuta Mkurugenzi wa
Manispaa ya Ilala ili kuzungumzia suala hilo
zilishindikana kwa kile kilichoelezwa na Katibu Muhutasi wake kwamba ana siku
maalum ya kumuona.
Ofisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala,
Tabu Shaibu alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa suala hilo, alijibu kwamba yupo kwenye kikao, hivyo
atume ujumbe mfupi wa simu. Pamoja na kutumiwa ujumbe huo tangu Jumatatu na
gazeti hili kuzidi kumfuatilia, alijibu suala hilo atampa injinia wa manispaa ya Ilala
afuatilie.
P amo j a n a a h a d i h i y o alipofuatiliwa zaidi aliahidi
kutoa namba za simu za injinia huyo kwa mwandishi wa gazeti hili ili awasiliane
naye, lakini hakufanya hivyo na alipopigiwa simu ilikuwa haipokelewi.Gazeti hili pia lilimtafuta Msajili wa
Bodi ya Wahandisi (ERB) Injinia Steven Mlote, ambapo alisema kwamba yuko mkoani
Arusha, lakini amewaagiza baadhi ya wafanyakazi kufuatilia jengo hilo mara moja.
Alipotafutwa tena ili atoe ufafanuzi
kuhusu jambo hilo,
Mlote alisema alikuwa hajapata taarifa zozote kutoka kwa wasaidizi wake, hivyo
alimtaka mwandishi wa habari hii kufika ofisini kwake ili akapate taarifa.
Licha ya mwandishi kufika ofisi za ERB
hakupata ushirikiano wowote na Mlote alipotafutwa tena simu yake haikupatikana.
Kwa upande wa Ofisa Uhusiano wa Wakala wa Majengo (TBA),
aliyejulikana kwa jina moja la Mariam alipotakiwa kuzungumzia jengo hilo, alitaka aandikiwe
maswali ili ayajibu kimaandishi
No comments:
Post a Comment