Na
Stella Aron
MWENYEKITI wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ameendelea kuliwekea ngumu
Jeshi la Polisi nchini kwa kukataa kukabidhi mkanda wa video unaoonesha tukio
la mlipuko wa bomu uliotokea kwenye mkutano wa CHADEMA, mkoani Arusha wakati wa
kuhitimisha kampeni za uchaguzi wa kata nne za madiwani.
Mbowe
aliripoti Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam jana kufuatia barua
aliyoandikiwa na jeshi hilo
likimtaka afike na kuwasilisha mkanda huo, anaodai anao. Akizungumza na gazeti
hili Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano wa CHADEMA, John Mnyika, alisema barua
hiyo ya Polisi ilikuwa ikieleza kuwa endapo atashindwa kuwasilisha mkanda huo
atakuwa ametenda kosa la jinai.
Mnyika
alisema Mbowe alienda mwenyewe Polisi akiwa na wakili wa CHADEMA, Peter
Kibatala na viongozi wengine wa chama. Mnyika alisema Mbowe aliwaambia Polisi
kuwa ushahidi wa mkanda huo hataukabidhi kwao, kwani wao ni miongoni mwa
watuhumiwa. "Amewaambia kama ni kosa la jinai libaki hivyo, lakini hawezi
kuwakabidhi mkanda huo kwa kuwa na wao ni miongoni mwa watuhumiwa,"
alisema Mnyika.
Kwa mujibu wa Mnyika, Mbowe
ameendelea na msimamo wake kuwa mkanda huo ataukabidhi kwa Tume ya Kijaji
itakayoundwa na si vinginevyo. Aliongeza kuwa baada ya maazimio ya Kamati Kuu
ya CHADEMA iliyokutana hivi karibuni, Mbowe alimwandikia Rais Jakaya Kikwete,
barua ya kumtaka aunde Tume ya Kijaji ya kuchunguza tukio hilo, lakini hadi sasa bado haijajibiwa.
Katika tukio hilo la mlipuko wa bomu watu wanne walifariki
na wengine wengi kujeruhiwa. Tangu wakati huo, Mbowe amekuwa akidai kuwa ana
ushahidi wa video wa tukio hilo,
lakini amekataa kuukabidhi kwa polisi kwa kile anachodai kwamba na wao ni
miongoni mwa watuhumiwa. "Kwa hiyo amewaambia Polisi kuwa bado jambo hilo ameandikiwa Rais
Kikwete na bado hajajibu hivyo hawezi kufanya hivyo," alisema Mnyika
akimnukuu Mbowe.
Alisema baada ya mazungumzo ya
kina kati yake na Polisi, walikubaliana kwamba Mbowe aeleze msimamo wake huo
kwa maandishi na kuwapelekea Polisi kesho na baada ya hapo watajua la kufanya.
Alisema baada ya mazungumzo hayo Mbowe aliondoka na yupo huru
No comments:
Post a Comment