30 July 2013

SERIKALI YASISITIZA KUWEKEZA KATIKA ELIMU



 Gladness Theonest na
Ester Maongezi
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo amesema kuwa Serikali ina jukumu la kuhakikisha inatoa elimu bora kwa wananchi wake na katika hali ambayo kila mtu anaweza kugharamia.Kauli hiyo ameitoa jana jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza udhamini wa maonyesho ya kwanza ya elimu kwa mwaka huu yatakayojulikana kama Vodacom Elimu Expo 2013.

Maonyesho yanayotarajiwa kuanza hivi karibuni na kupewa maudhui ya ‘Elimu Bora ndio Tegemeo la watoto wetu, Tuijenge kwa Pamoja’.Mulugo alisema kuwa, wananchi walio wengi wanaangalia ubora wa elimu na si kiwango cha ada na ndio maana katika kipindi cha nyuma wengi wao walikuwa wakipeleka watoto wao kupata elimu nje ya nchi.
Alisema kuwa, serikali na wadau mbalimbali wa elimu nchini wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kujenga shule na kuweka huduma zote, hivyo kuna haja ya kugharamia huduma hizo ili huduma bora ya elimu iweze kupatikana nchini.“Kwa kuliangalia hilo serikali inatafuta jinsi ya kutoa ada elekezo kwani elimu si biashara bali ni huduma kwa kuweka kiwango fulani ambacho kitafanya kila mwananchi aweze kukimudu kwa kuhakikisha elimu bora inapatikana kwa wananchi wote na kwa gharama nafuu,” alisema Mulugo.
Naye Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa Vodacom, Kelvin Twissa alisema kuwa matumaini ya Vodacom Elimu Expo yatasaidia kusuluhisha changamoto mbalimbali zinazokabili sekta ya elimu nchini.Twissa alizitaja moja ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na kulipa ada ya shule kwa kupanga foleni jambo ambalo linaonyesha kupoteza muda mwingi katika mistari mirefu ya benki.
“Ni jambo la kusikitisha kabisa kuchelewa kulipa ada ya shule kwa sababu ya foleni zilizopo katika benki zetu, Kampuni ya Vodacom imekuja na njia ya kitatua changamoto hii na sasa kuna uwezekano wa kulipa ada ya shule kupitia M-Pesa , hivyo tunawasihi wadau wa elimu wanaomiliki shule kuanza kutumia huduma hii,” alisema Twissa.
Naye Mkurugenzi wa Elimu Expo Solution Tanzania Limited, Joel Njama aliwataka wadau wa elimu nchini kujitokeza kwa wingi katika maonyesho hayo na kusaidia elimu katika nyanja tofauti kutokana na elimu kuwa ndio ufunguo wa maendeleo katika Taifa hili kubwa la Tanzania.
Maonyesho hayo ya siku tatu yanatarajia kufanyika kuanzia Agosti 30, mwaka huu na yamedhaminiwa na makampuni ya Vodacom Tanzania na Elimu Solutions Tanzania Limited.Aidha, yamelenga kuwahusisha wadau wa elimu katika kuangalia mi a n y a i l i y o p o , k u g u n d u a changamoto na kutafuta suluhisho la kupeleka elimu bora kwa Watanzania kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment