Na Rehema Mohamed
ALIYEKUWA Katibu wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) Mkoa wa Dodoma Kapteni mstaafu, John Barongo amesema mapendekezo ya
kubadilisha Muungano uwe wa Serikali tatu ni kichekesho hasa kwa kipindi hiki
ambapo Afrika inafikiria kuwa na serikali moja.
Kapteni Barongo
aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa
habari kuhusu rasimu ya Katiba Mpya na maoni mbalimbali yanayotolewa kuhusu
muundo wa Katiba Mpya.Kapteni Balongo
alisema, wazo la kuwepo kwa serikali tatu ni la baadhi ya viongozi wachache
wanaotaka madaraka huku wengine wakizungumzia kuundwa kwa Katiba ya Tanganyika
ili wapate uongozi badala ya kuzungumzia matatizo ya wananchi.
Pamoja na hilo,
Kapteni Balongo alikiri kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar una matatizo na
kusema kuwa hizo ni changamoto ambazo zinahitaji ufumbuzi wa pamoja na si kuwa
na serikali tatu.Alisema, huko nyuma
kuna baadhi ya nchi zilijaribu kuwa na muundo wa serikali tatu na kushindwa
kuziendeleza huku akitolea mfano wa nchi ya Egypt na Syria ambazo ziliwahi
kuunda Shirikisho la Syria (United Arab Republic) ambapo mwezi Septemba mwaka
1961 Mkuu wa Majeshi wa Syria alijiondoa katika shirikisho hilo na ukawa mwisho
wa muungano huo.
"Nchi nyingine
ni Mali na Senegal ambapo wao waliunda Mali Federation wakati huo Mali ikiitwa
French Sudan, akachaguliwa Modibo Keita akawa Rais wa serikali hizo tatu na
matokeo yake Rais wa Senegal wakati huo Leopold Sedar Senghor alijiondoa na
ukawa mwisho wa shiririkisho hilo,"alisema Kapteni Barongo
Alisema kuwa,
Watanzania wanatakiwa wajifunze kutoka katika nchi hizo kwani kuwepo na
serikali hizo ni mzigo kwa wananchi kuhudumia marais wa serikali tatu hasa kwa
wakati huu ambapo uchumi wa nchi si mzuri.Alisema kuwa, ni bora
nchi ikabaki na serikali mbili kama ilivyo sasa na kisha kutatua mambo
yanayokwamisha Muungano kuliko kuruhusu tatu ambazo zinaweza kuongezeka na kuwa
nne kutokana na mapendekezo ya watu.
Hata hivyo, alitaka
suala la ardhi lisiwe sehemu ya Muungano kwa sababu Wazanzibar wengi wanakuja
Tanganyika na kujenga ambapo kwa Watanganyika inakuwa vigumu kupata ardhi
Zanzibar.Akizungumzia mchakato
wa Katiba mpya alisema, hakuna ulazima wa nchi ikawa na Katiba Mpya ifikapo
mwaka 2015 na badala yake yaangaliwe mapungufu yaliyopo katika katiba ya sasa
na kufanyiwa marekebisho.
"Mapungufu
katika katiba ya sasa yapo ila kinachotakiwa ni kubainisha mapungufu hayo na
kuyafanyia kazi na si kuiga nchi za jirani kama Kenya walivyobadili katiba yao,
nadhani tungekuwa na katiba nzuri zaidi miaka 10 kutoka sasa,"alisema.
Katika hatua
nyingine, Kapteni Barongo amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kusimamia, amani,
mshikamano na kupambana na ufisadi wa kila aina,kuwahudumia wananchi katika
kupata haki zao na kuwakataa viongozi wanaotumia vitu hivyo kwa masilahi yao.
Alisema kuwa,
wananchi wanajua nani anayefaa kuongoza nchi na kwamba Rais wa nchi hii anaweza
kutoka chama chochote isipokuwa rais bora anatokea CCM.
Alisema
kuwa, viongozi wa CCM lazima wabadilike na kuachana na kuongoza kwa mazoea
ikiwa ni pamoja na kufahamu aina ya rais anayetakiwa kusimama mwaka 2015
asiyekuwa wa kununua watu bali wananchi wampende wenyewe
No comments:
Post a Comment