Na Rachel Balama
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais
Mazingira wa zamani, Arcado Ntagazwa (65) na wenzake wawili wanaokabiliwa na
shtaka la kujipatia mali ya zaidi ya sh.milioni 74 kwa njia ya udanganyifu
wamepatikana na kesi ya kujibu.
Akitoa uamuzi
huo, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu Gene Dudu alisema kuwa, kwa mujibu wa
ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka mahakamani hapo unaonyesha kwamba
washtakiwa wana kesi ya kujibu.
"Mahakama
imeona washtakiwa wote wana kesi ya kujibu kutokana na ushahidi wa upande wa
Jamhuri hivyo kila mtu atajibu shtaka mahakamani", alisema Hakimu huyo.
Katika kesi
hiyo, upande wa serikali unaongozwa na Wakili Charles Anindo ambapo ulikuwa na
mashahidi watano.
Washtakiwa wengine
katika kesi hiyo ni Dkt. Webhale Ntagazwa (29) na Seneta Miselya (60).
Washtakiwa hao kwa
pamoja wanadaiwa kujipatia mali ya zaidi ya sh.milioni 74 kwa njia ya
udanganyifu.
Aidha, walidaiwa kuwa
Oktoba 22, 2009 maeneo ya Mikoroshini Msasani katika Wilaya ya Kinondoni,
washtakiwa kwa nia ya udanganyifu walijipatia kofia 5,000 na fulana 5,000
kutoka kwa Noel Severe zenye thamani ya sh. milioni 74.
Ilidaiwa kuwa
washtakiwa hao walimdanganya Severe kuwa bidhaa hizo wangezilipa baada ya mwezi
mmoja tangu kupewa mzigo huo, jambo ambalo hawakulitekeleza.
Hata hivyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 2, mwaka huu
ambapo washitakiwa wataanza kujitetea.
No comments:
Post a Comment