05 July 2013

RC AWAVAA WACHOMAJI MISITU


 Na Said Hauni, Lindi
MKUU wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila amewataka wananchi wa Kanda ya Kusini kutunza mazingira ikiwemo kuacha tabia ya uchomaji moto na ukataji wa miti ili kuepusha nchi kugeuka jangwa.
Mwananzila alitoa rai hiyo jana wakati akifungua warsha kwa wadau wa hifadhi ya misitu (Mjumita na Mkuhumi) iliyofanyika mjini Lindi.
Akifungua warsha hiyo iliyojumuisha washiriki wa Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma alisema misitu ina mchango mkubwa ikiwemo kujitengenezea chakula chake na kunyonya hewa ukaa kwa kutoa hewa safi na kuhifadhi hewa chafu katika udongo mara mbili zaidi ya kiwango chake katika dunia.

Mkuu huyo wa mkoa alisema tabia ya ukataji miti ovyo mara nyingi imekuwa ikichangia uharibifu wa mazingira na hivyo kuongezeka kwa hali ya joto kali inayosababisha madhara kwa nchi kutokana na kukosekana kwa mvua ya uhakika.
Mwananzila alisema iwapo mazingira hayatalindwa upo uwe z e k a n o mk u bwa wa kuongezeka kwa joto, majangwa, vimbunga, mafuriko, bahari kuendelea kujaa maji kutokana na kuyeyuka kwa barafu.
Alisema Serikali kwa upande wake imeipa kazi Mjumita katika kutoa elimu na kuhamasisha jamii juu ya mpango wa Mkuhumi katika ngazi za vijiji na Taifa kwa lengo la kujenga uelewa na kupata maoni ya wananchi juu ya upashanaji habari pale utaratibu wa biashara ya hewa ukaa utakapokuwa tayari katika ngazi za kimataifa.
Pia aliyaagiza mashirika ya Mjumita, Mkuhumi, taasisi nyingine na jamii yaliyopo ukanda wa Kusini yafanye kazi kwa ushirikiano wa pamoja ili kuleta mafanikio kwa kanda nzima ya Kusini na Taifa kwa ujumla.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Lindi alisema hewa ukaa huzalishwa zaidi ma nchi za mataifa makubwa yaliyoendelea kutokana na viwanda vyao huku nchi za Afrika zikizalisha Oksijeni ya kwenye miti yao ya mali asili.
Kwa upande wake Mshauri wa masuala ya misitu mkoani humo, Mwinjuma Mkungu alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwapa elimu wadau, watendaji wa Serikali ngazi za halmashauri na vijiji ili kulinda mazingira ikiwemo misitu.
Aidha, alisema semina kama hiyo ilishafanyika katika Kanda ya Nyanda za Juu (Mbeya) Kanda ya Kati (Dodoma) na Kaskazini (Arusha) na kujumuisha washiriki 243 na kuongeza hadi mwisho wa semina hiyo itakuwa imehusisha washiriki 343 na kuongeza kuwa semina nyingine itafanyika katika Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment