Na
Elizabeth Joseph, Dodoma
MWANASHERIA Mkuu wa
Serikali (AG) Jaji Frederick Werema, amewaonya na kuwataka wapelelezi nchini
kuacha tabia ya kubambikiwa kesi watu wakati hawana hatia yoyote.Jaji Werema, alitoa
onyo hilo wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Mawakili wa Serikali Wafawidhi
na Wakuu wa Upelelezi wa Mikoa uliofanyika jana, mjini Dodoma.
Alisema kumekuwa na
tabia ya uonevu wa kuwabambikia kesi watu, vitendo ambavyo amevipinga vikali
kuwataka kutumia weledi wakati wa kumkamata wahalifu.“Tusitumie nguvu
kumkamata mhalifu wala kulipa kisasi kwa kuwabambikiwa kesi pamoja na kumkamata
mtu kama hamna ushahidi wa kutosha, kwani kufanya hivyo kutaleta uhusiano mzuri
na wananchi,” alisema Jaji Werema.
Aliwataka wanasheria
na wakuu wa upelelezi hao kuhakikisha upelelezi na ushahidi wanaoutaka
unapatikana haraka pamoja na kuwafahamisha washtakiwa hatua waliyoifikia na
haki zao kisheria, ili kuleta imani kwa watu wanaowatumikia pamoja na kuondoa
manung’uniko miongoni mwao.
Jaji Werema pia
aliwataka wakuu hao kufuata maadili ya kazi zao, ikiwa ni pamoja na kutunza
kumbukumbu na majalada ya kesi mbalimbali, kwani ni wajibu wao kuyalinda kwa
kuyahifadhi katika hali nzuri.
Mbali na hilo,
alikemea vitendo vya baadhi wa mawakili wafawidhi na wakuu wa upelelezi kuacha
tabia ya kuuza kesi kwa watu kwa kupokea rushwa jambo ambalo linavunja miongozo
ya kazi wanayosimamia
No comments:
Post a Comment