SHEREHE ya kuzaliwa kwa Rais wa
Kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, zinafanyika leo hafla itakayoambatana
na shughuli za kusaidia wasiojiweza ndani ya jamii ulimwenguni kote leo.
Leo
Mandela anaadhimisha kutimiza miaka 95 ingawaje bado yuko mahututi katika
hospitali mjini Pretoria, Afrika Kusini.
Watu
mbalimbali wa kujitolea watatumia dakika 67 kwa miradi tofauti ya kuboresha
maisha, kila dakika ikiwa inasimamia kila mwaka ambao amekuwa akiwatetea watu
maishani mwake
.
Hata
hivyo, kulazwa kwake hospitalini na pia migogoro ndani ya familia yake
imeathiri uchangamfu wa siku ya leo wa kuzaliwa kwake.
Shirika
la Umoja wa Mataifa mwaka 2010 lilitangaza siku ya kuzaliwa kwake Mandela
ambaye ni mshindi wa Tuzo ya Nobel, kuwa ni ya kuadhimishwa kila mwaka kama
njia ya kuwahimiza watu kote ulimwenguni kufanya angalau saa moja ya mambo
mema.
Watu mashuhuri
na pia wanaosifika duniani wamekuwa wakisaidia juhudi hizo za kukumbuka miaka
67 ya juhudi zake Mandela.
Leo watoto
katika shule zilizopo Afrika Kusini wataanza kwa kumwimbia mkongwe huyo, huku
watu wanaosifika wakijitolea kupiga rangi shule, kuwapatia nguo watoto maskini.
Shule yenye jina lake inatarajiwa kufunguliwa kama
kumbukumbu za shujaa huyo. Nchini Amerika, miji 17 pia imepanga kufanya hafla
tofauti kwa ajili ya kumbukumbu ya kuzaliwa
No comments:
Post a Comment