WAZIRI wa nchi
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, C e l i n a K o m b a n i
amesema sasa umefika wakati mwafaka kwa Manispaa ya Morogoro kuwa jiji baada ya
kukidhi vigezo muhimu ikiwemo masuala ya usafi na miundombinu ya barabara kuwa
katika kiwango cha lami.
Kombani alisema hayo hivi karibuni
wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya Serikali za Mitaa yanayoadhimishwa kitaifa
katika Manispaa ya Morogoro ambapo alisema akiwa Waziri wa Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa aliwahi kukataa maombi ya Manispaa hiyo kuwa jiji kutokana na
kushindwa kukidhi vigezo mbalimbali ikiwemo usafi.
Kwa sasa niko tayari kuwa mpiga debe ili
kuhakikisha Manispaa hiyo inakuwa jiji, kwanza ina sifa stahili, mwaka huu
imeshika nafasi ya tatu kitaifa kwenye suala la usafi, barabara za lami
zimeongezeka," alisema Waziri Kombani
Alisema kuwa Manispaa ya Morogoro
isitafute mchawi kwa wakati ule kutoruhusiwa kuwa jiji kwani vigezo vingi
havikuwa vimetimia lakini kwa sasa kila kitu kinaonekana wazi, hoteli nzuri,
kwa wakati wake manispaa ilishika nafasi ya 13 kiusafi.
Alisema pia Manispaa ya Morogoro iko
katikati ya kuelekea mikoa mbalimbali na nchi za jirani, hivyo kuwa na hadhi ya
jiji kutasaidia kuboresha zaidi utoaji wa huduma mbalimbali.
K o m b a n i a l i y e k u w a
akimwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, alisema siku ya
Serikali za Mitaa ni muhimu kwa mamlaka za Serikali za Mitaa kama watekelezaji
wakuu wa mipango ya maendeleo ya taifa na hutumia siku hiyo kujipima kwa
kuangalia walikotoka, walipo na wanakokwenda katika utoaji wa huduma bora kwa
wananchi.
A l i t u m i a n a f a s i h i y o
kuwakumbusha watendaji wa Serikali za Mitaa, kuwashirikisha wananchi katika
utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, ili wananchi waweze
kutambua kuwa Serikali inatambua na kuthamini juhudi zao na kutoa hamasa kwao
katika kusimamia vyema miradi hiyo.
Kauli
mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni Amani, Uadilifu na uwajibikaji ni
nyenzo muhimu kwa mchakato wa katiba mpya.
No comments:
Post a Comment