Na Rachel Balama
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam
imeahirisha kesi ya ubadhirifu inayomkabili Askofu Mkuu wa Kanisa la Full
Gospel Bible Fellowship (FGBC), Zakaria Kakobe hadi Septemba 26, mwaka huu
kutokana na Jaji anayesikiliza kesi hiyo kuumwa.
Kesi hiyo
iliahirishwa jana na Msajili wa Mahakama Kuu kutokana na Jaji Iman Abood
anayesikiliza kesi hiyo kuumwa na kutofika mahakamani.Upande wa walalamikaji unawakilishwa na Wakili Barnabas Luguwa, upande
wa utetezi unawakilishwa na Wakili Miriam
Majamba.
Kesi hiyo namba
79/2011 ilifunguliwa Mei 26, mwaka jana na wachungaji watatu wa kanisa hilo; Deuzidelius
Patrick, Angelo Mutasingwa na Benedict Kaduma.Hata hivyo,
baadaye Mc h u n g a j i K a d u m a alilazimika kujitoa kutokana na ushauri wa
ndugu na daktari, baada ya kupata ajali na kulazimika kufanyiwa u p a s u a j i
mk u bwa wa kichwa.
Baadaye, msimamizi wa kanisa hilo
wilayani Liwale, mkoani Lindi, Mchungaji Ignas Innocent aliwasilisha maombi
kutaka kujiunga katika kesi hiyo huku akidai ameamua kupigania haki na
kwamba, kuna mambo ambayo anataka kuyaweka wazi.
Wa c h u n g a j i h
a o wanamtuhumu Askofu Kakobe licha ya mambo mengine, kwa ubadhirifu wa mali na
fedha zaidi ya sh.bilioni 14 na ukiukwaji wa katiba ya kanisa hilo.Awali, Askofu Kakobe
kupitia kwa wakili wake, Miriam Majamba aliwawekea p i n g ami z i l a a w a l
i walalamikaji hao akidai hawana haki ya kumfungulia kesi, lakini juhudi zake
ziligonga mwamba baada ya mahakama kulitupilia mbali.
Katika pingamizi lake
hilo, licha ya kudai walalamikaji
hawana haki ya kisheria kumfungulia kesi, kwamba si wachungaji wa kanisa hilo kwani walishafukuzwa
tangu mwaka 2010.
No comments:
Post a Comment