26 July 2013

GHOROFA HATARI

  • MAPYA YAIBULIWA

Na Mwandishi Wetu
SAKATA la jengo la Golden Plaza lililopo Mtaa wa Agrey na Indira Gandh jijini Dar es Salaam limezidi kuchukua sura mpya kutokana na wapangaji wa jengo hilo kuonesha kasoro kubwa zilizopo kwenye jengo mbali na nyufa zinazoashiria kwamba linaweza kuanguka wakati wowote.Akizungumza na gazeti hili mmoja wa wapangaji katika jengo hilo (jina tunalo) alisema jengo hilo limejengwa na taasisi mbili (majina tunayo).

Alisema jengo hilo lina wapangaji wanaolitumia kama ofisi na makazi ya watu zaidi ya 70. Alisema ghorofa mbili ndizo zinazotumika kwa ajili ya maduka na ofisi.Alisema yeye ndiye mpangaji wa kwanza katika jengo hilo na amekuwa akipeleka malalamikahusika bila hatua kuchukuliwa.
"Tumelalamika matatizo ya jengo hili lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa," alisema.
Mpangaji mwingine (jina tunalo) alisema jengo hilo lina matatizo mengi yakiwemo ya baadhi ya vifaa vilivyotumika kulijenga kuangua chini.Majira ilishuhudia baadhi ya vyumba vya wapangaji vikiwa na miinuko ambapo marumaru zilizowekwa chini badala ya sakafu zimebanduka na kusababisha miinuko.
Mbali na hilo pia katika ghorofa ya pili ya jengo hilo imejaa maji kutoka kwenye mabomba yanayotoka ghorofa ya juu na kusababisha maji kutuama.Mmoja wa wapangaji alisema hali ni mbaya katika baadhi ya ghorofa za jengo hilo kutokana na kuwa na nyufa za kutisha. "Kuja kufika kwenye ghorofa hizo labda mje na polisi ndipo mjionee hali ilivyo ndani," alisema mpangaji huyo kwa sharti la jina lake kutochapishwa gazetini.
Baadhi ya wananchi waliokuwepo karibu na jengo hilo, walisema kwa sasa lazima mamlaka husika zifanye kazi kwani inaonekana jengo hilo halikujengwa kitaalamu.Walisema ukiliangalia jengo hilo utaona nyufa nyingi kwani kuna marumaru zimebanduka ukutani na kuanguka na hata rangi za ukutani zinamechakaa zina maji yanayopenya kutoka ghorofa za juu.
"Ni vyema Serikali ikawafuatilia wahusika na kulifanyia ukaguzi wa kina jengo hili kabla halijaleta madhara kwani wataalamu hawafiki kwa ajili ya ukaguzi na hata kama wakija hakuna majibu wala taarifa wanazotoa kwa watumiaji wa jengo hilo," alisema mmoja wa wananchi wenye biashara eneo hilo.
Licha ya majira kufanya jitihada kwa siku tatu ili kupata ufafanuzi wa jengo hilo kutoka Manispaa ya Ilala na Bodi ya Usajili wa Waandisi (ERB) lakini wahusika wa sehemu hizo wamekuwa kimya

3 comments:

  1. Jengo lingine tena la NHC yenye utata.

    ReplyDelete
  2. mmh jamani my Engeneer mko wpi?mmesomea nini vyuoni?mbona mnataka kuuwa wananchi wetu kwa ajili ya tamma zenu za hela, mungu awasamehe kwa ababu hamui mlitendalo

    ReplyDelete
  3. Hatari sana.serikali lazima ichukue hatua kali

    ReplyDelete