15 May 2013

Sweden kuisaidia TANESCO kufua umeme

Na Darlin  Said
 kAMPUNI za kufua umeme kutoka nchini Sweden, zipo katika mchakato wa kuzalisha umeme kwenye vyanzo mbalimbali baada ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO), kutokidhi hitaji la kutoa huduma hiyo kwa wananchi wengi.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akiwakaribisha wawekezaji hao na kuongeza kuwa, lengo la Serikali ni
kuiboresha TANESCO ili iweze kutoa huduma bora.
 Alisema tangu kuanzishwa kwa shirika hilo mwaka 1961 ni asilimia 21 tu ya Watanzania waliopo mijini na asilimia saba waliopo vijijini ambao ndiyo wanaopata huduma ya umeme.
“Kimsingi hali hii inasikitisha, tumegundua kuwa TANESCO peke yao hawawezi kutoa huduma ya umeme kwa Watanzania wenye hitaji hilo hivyo wataendelea kuumia,” alisema.
Prof. Muhongo aliongeza kuwa, Serikali imewakaribisha wawekezaji hao kwa sababu haina fedha za kuwekeza katika sekta ya nishati ili kusambaza huduma ya umeme.
“Pato la Taifa ni dola za Marekani bilioni 28 ambazo tukizigawa, kila Mtanzania atapata sh. 6,000 hivyo lazima tutegemee wawekezaji ili tuweze kujikomboa,” alisema.
Alisema wawekezaji hao mbali ya kufua umeme nchini, pia watatekeleza miradi mbalimbali, k u b o r e s h a mi u n d omb i n u , kusambaza umeme vijijini na kupunguza upotevu wa umeme.
Aliongeza kuwa, vyanzo vyote vya umeme nchini vingeweza kuzalisha umeme wa megawati 1,438.24 lakini miundombinu iliyopo hata kama umeme huo ungezalishwa, wangeshindwa kuusambaza kutokana na ubovu wa miundombinu ambao hupoteza asilimia 23.4 ya umeme.
Alisema kampuni hizo zitafua umeme kupitia upepo, miamba, kinyesi cha wanyama, maji, jua na kusisitiza kuwa ni ndoto ya mchana kuitegemea TANESCO izalishe umeme kupitia vyanzo hivyo.
Kwa upande wake, Balozi wa Sweden nchini, Bw. Gunnar Oom, alisema wameamua kuwekeza Tanzania baada ya kuona misaada pekee wanayotoa haiwezi kuongeza
 kasi ya maendeleo.
Alisema kupitia uwekezaji huo, utasaidia kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kiuchumi pamoja na kubadilishana uzoefu.
“Kupitia uwekezaji huu, pia utasaidia kubadilishana bidhaa kwa kununua zilizopo Tanzania kwani nchi nyingi za Afrika zinategemea sana kuuza mafuta, madini na mazao ya chakula nje,” alisema.

No comments:

Post a Comment