16 May 2013

Madiwani wawasimamisha kazi watumishi kwa ubadhirifu

Na Queen lema, Arusha


 BARAZA la Madiwani Halmashauri ya ArushaVijijini,WilayayaArumeru limewa simamisha kazi watu mish iwatano wa halmashauri hiyo kwatuhuma za ubadhirifu.
Watumishi haowanakabiliwanatuhuma ya ubadhirifuwash.milio ni 56 6,654,173zilizoto lewa kwaajili yakujenga v yumbavyam ada rasaka tikabaadhi ya shule za sekondari zahalm ashaurih iyo.
Mwenyekiti wa HalmashauriyaArusha,Bw.SaimonSaning'oakitangaza uamuzi huo jana, a lisemamhusikamkuu katikakatikashauri hilo ni wasaid izi wake watatu .
Alisemawatumishi hao wamesimamishwa kupishauchunguzi.Aliongezakuwa wamebainikabaada yaMku rugenzi Mtendaji aliyehamishiwa katika Halmashauri hiyo kumuagiza Mkaguzi
wandanikatikahalmashauri hiyo, Bw. Jackson Laizer, kufanya ukaguzi.
Mwenyekiti huyo alisema wamebaini wizi wa fedha hizo Februari, mwaka huu na kuwa mchezo ulianza kufanyika Desemba mwaka uliopita.
Alisema kuwa, fedha hizo hazikupelekwa shuleni kama ilivyoelekezwa.
Mkaguzi huyo anadaiwa kubaini kuwa hati za malipo ziliandaliwa nje bila mfumo funganishi wa EPICOR na malipo kufanyika bila hidhini ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, malipo kufanyika bila vifungu vya bajeti na hati za malipo zilizoandikwa kwa mkono.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Arusha kwa sasa, Fedelist Lumato akizungumzia tukio la kusimamishwa kwa watumishi hao, alisema kuwa watumishi hao watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

No comments:

Post a Comment