16 May 2013

CCM yaibana serikali uchomaji makanisa

Na Salim Nyomolelo


 MBUNGE wa Fuoni kwa tiketi ya CCM, Bw.Said Mussa Zuberi, ameshangazwa na wabunge kupitisha bajeti za wizara mbalimbali, lakini fedha hizo hazipelekwi kama zinavyoidhinishwa.
Alitoa kauli hiyo mjini Dodoma wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2013/2014. Alisema inashangaza wabunge kupitisha bajeti, lakini
fedha zinazotolewa ni kidogo na vilevile hazipelekwi zote kwenye wizara husika.
 Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Makao Makuu ya CCM,jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Bw. Nape Nnauye, alisema mkutano wa Kamati Kuu ya CCM uliofanyika hivi karibuni, umeitaka Serikali kuhakikisha mizizi inang’olewa ili kukomesha matukio ya aina hiyo.
Nape alisema kuwa CCM i m e r i d h i s h w a n a h a t u a zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi wakati wa tukio hilo. Alisema Kamati Kuu, ililaani matukio hayo kutokana na kuwa yanavuruga amani, upendo na umoja wa Watanzania.
“Kamati Kuu imeishauri Serikali kuongeza kasi kuwasaka na kung’oa mzizi huo ili kukomesha vitendo vya namna hiyo,” alisema, Bw. Nape
Hata hivyo, Bw. Nape alisema Mei 18 na 19 mwaka huu Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, atakutana na wabunge wa chama chake pamoja na sekretarieti ya chama ili kupata maoni ya wabunge pamoja na kushauriana katika nyanja mbalimbali za maendeleo.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari, Bw. Nape alisema kuwa miongoni mwa ajenda zitakazozungumzwa ni pamoja na utekelezaji wa ilani ya chama na mwenendo wa maendeleo pamoja na kuweka mikakati thabiti ya maendeleo.
“Kikao kitakuwa kati ya mwe n y e k i t i , wa b u n g e n a sekretarieti ambayo ndiyo wamiliki wa ilani inayotekelezwa,” alisema.
Alisema kuwa baada ya kikao hicho na wabunge hao, Kamati Kuu ya CCM itakutana tena Mei 20 na 21 ili kujadili mambo yatakayoongelewa katika kikao cha wabunge.

No comments:

Post a Comment