20 June 2012

Tamasha la Supa5 sasa kufanyika Mwanza



Na Mwandishi Wetu

MATAMASHA ya kuitambulisha huduma Airtel Supa5 utaendelea tena mwishoni mwa wiki ambapo safari hii itakuwa ni zamu ya jiji la Mwanza ambalo wakazi wake watapata burudani katika viwanja vya wazi vya Furahisha.

Akizungumzia tamasha hilo jana  la kuitambulisha Supa5 jijini Mwanza Ofisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde alisema lengo la kuunganisha utambulisho huu kwa burudani ni kuwavutia vijana na wateja wengi kuhudhuria na kujifunza faida za Supa5 ili waitumie zaidi.

Alisema tamasha hilo litafanyika kwa siku mbili mfululizo ambapo Jumamosi watatoa fursa kwa wasanii chipukizi kujitokeza kwa wingi kuonesha vipaji vyao sambamba na kupata huduma ya Airtel Supa5.

Ofisa huyo alisema Jumapili itakuwa uzinduzi kamili ambapo wasanii wakongwe watatoa burudani, akiwemo Juma Nature na kundi zima la Wanaume Halisi, Mwasiti 'Soja' na Roma Mkatoliki watatoa burudani kwa wateja watakaohuduria tamasha hilo ambalo ni la bure.

Matinde alisema lengo la huduma hiyo ni kuhakikisha Airtel inatimiza dhamira yake iliyojiwekea ya kufikisha na kupunguza gharama za mawasiliano nchini kote bila kuwasahau vijana na wanafunzi kunufaika kwa kupata internet bure wakati wa usiku, kutuma sms bure na faida nyingine nyingi.

Huduma ya Airtel Supa5 ilizinduliwa hivi karibuni jijini Dar es salaam na baadaye kuendelea na matamasha katika mikoa ya Dodoma, Morogoro, Iringa na Arusha.

No comments:

Post a Comment