13 June 2012

Msondo, Sikinde uso kwa uso Juni 14



Na Daud Magesa, MWANZA

BENDI mbili kongwe za Muziki wa Dansi zenye upinzani wa jadi, DDC Mlimani Park (Sikinde) na Msondo Ngoma, zinatarajia kutoa burudani katika maadhimisho ya sherehe za miaka mitano tangu kuanzishwa kwa  klabu ya starehe ya Villa Park Resort.


Sherehe hizo zitahusisha michezo ya soka, muziki wadansi, taarabu na disco zitafanyika kuanzia Juni 14 hadi 16, mwaka huu jijni.

Akizungumza na gazeti hili jana kuhusu sherehe hizo, Meneja wa hoteli ya Villa Park Resort, Shijani Mtunga, alisema sherehe hizo zimelenga kuwakumbuka wadau wanaofanya nao biashara na kujumuika nao ili kurudisha fadhila kwao.

Alisema kutokana na wadau hao kuwaunga mkono, ili kusherehekea vizuri wamewaandalia burudani mbalimbali za soka, muziki wa dansi, taarabu na disco kwa kila mtu.

Alisema wapenzi wa muziki wa dansi, watapata burudani ya muziki huo kutoka kwa Msondo Ngoma na Sikinde, zitakapopambana Ijumaa, zikisindikizwa na bendi mwenyeji ya Super Kamanyola, ambapo Jumamosi itakuwa ni mapumziko na fainali itafanyika Jumapili.

Alisema ufunguzi wa bonanza hilo utafanyika Alhamisi kwa msanii, Jokha Kassim maarufu kama Kanga Moko, atachengua kwa kutoa burudani ya muziki wa taarabu na Ijumaa kutakuwa na disko.

“Bonanza hili la miaka mitano ya Villa Park, si kucheza tu bali pia kufanya mazoezi ili kujenga afya.Kauli mbiu yake ni kula ni lazima, michezo ni afya," alisema Mtunga.

No comments:

Post a Comment