19 June 2012
Bonanza vyuo vikuu lafana Dar
Na Victor Mkumbo
BONANZA la michezo mbalimbali la Vyuo vya Elimu ya Juu vya Dar es Salaam lililofanyika juzi lilikuwa kivutio kwa wadau waliojitokeza.
Bonanza hilo lililoshirikisha vyuo saba ambalo lake lilikuwa kuibua vipaji lilifanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ardhi, Dar es Salaam.
Vyuo vilivyoshiriki bonanza hilo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM), Chuo Cha Ustawi wa Jamii, Chuo Kikuu cha Biashara (CBE), Chuo cha Ualimu (DUCE) na Chuo Kikuu cha Kampala (KIU).
Katika bonanza hilo ambalo lilifanyika kwa mwezi mmoja lildhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Tanzania Breweries (TBL) kupitia kinywaji chake cha Grand Malt, ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bernad Marcelline, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Akizungumza mara baada ya kumalizika bonanza hilo, Marcelline alisema michezo hiyo imefanikiwa kuimeibua vipaji vya wanafunzi wa vyuo hivyo katika michezo mbalimbali.
Alisema vijana hao hawana budi kujikita katika fani mbalimbali za michezo, kutokana na kuwa michezo ni ajira.
Marcelline alisema washindi walioshinda kwenye michezo mbalimbali wanatakiwa wawe changamoto kwa kuwashawishi wenzao kuingia katika fani ya michezo.
Naye Meneja wa Grand Malt Consolata Adam, alisema wanatarajia kuendelea kudhamini bonanza hilo katika mikoa yote yenye vyuo vikuu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment