17 May 2012
'Wakuu wa Wilaya simamieni mfumuko wa bei Dar'
Na Heri Shaaban
Dar es Salaam
WAKUU wa Wilaya za Dar es Salaam wameagizwa kusimamie mfumuko wa bei ya vyakula katika masoko ya wilaya zao.
Agizo hilo limotolewa na Mkuu wa mkoa huo Bw.Meck Sadik mara baada kuwapisha wakuu wa wilaya zake.
Bw.Sadik alisema kuwa kutokana na mfumuko wa bei katika bidhaa,anawagiza kutoa kipaumbe kushughulikia suala hilo kwa kufanya ziara katika masoko na kuangalia bei ya vyakula.
Alisema kuwa katika masoko ya mkoa huo bei ya unga sembe kilo moja inauzwa shilingi 1200 hadi 1400 jambo ambalo wananchi wengi wanashindwa kumudu ukali wa gharama za maisha na kulazimika kula mlo mmoja kwa siku.
"Serikali imeshasambaza mahindi mengi kutoka katika Ghala la Serikali kwa kuwapa wafanyabiashara wakubwa kama Bakhresa hivyo kwa sasa unga wa sembe utauzwa kwa bei ya shilingi 800 kwa kilo,"alisema Bw. Sadik.
Aliwataka wakuu wa wilaya hizo wawe na utaratibu ya kutembelea masoko na kuangalia bei za bidha zinazopanda mara kwa mara.
Alisema wafanyabiashara wote watakaouza unga sembe kwa bei kubwa badala ya bei ya serikali watachukuliwa hatua huku leseni zao zikikamatwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment