06 February 2012

SERIKALI imekubali kutekeleza masharti makuu yaliyotolewa na wafanyakazi kabla ya Mei Mosi lengo ni kuzuia mgomo usio na kikomo unaotarajiwa kufanywa Mei Mosi mwaka huu.

Kaimu Katibu Mkuu wa TUCTA Bw. Nicholas Mgaya alisema, kikao chetu si cha kudhoofisha jitihada za maandalizi ya mgomo kama baadhi ya watu wanavyodhani.

"Tumekutana nia ni kuzuia huu mgomo kwa serikali kutekeleza masharti yetu. Madai yetu makuu ni matatu, nyongeza ya mishahara, kupunguzwa kwa kodi ya mapato inayokatwa kwenye mishahara na mafao bora ya uzeeni kutoka kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii," alisema

No comments:

Post a Comment