27 January 2012

SERIKALI, MADAKTARI WAFIKISHANA PABAYA.

Serikali, madaktari wafikishana pabaya


*Sasa wapashana kupitia vyombo vya habari pekee
*Wagonjwa wataabika, ndugu wahaha kuwahamisha
*Watangaza athari za mgomo ndani ya siku 12


 Anneth Kagenda na Rehema Maigala

WAKATI afya za wagonjwa wanaotibiwa katika

hospitali mbalimbali nchini zikizidi kudhoofika kwa

kukosa matibabu, kwa mara nyingine tena madaktari

na serikali jana wameendelea kutunishiana misuli,

hali inayodhihirisha kuwa muafaka wa sakata hilo

bado kitendawili.

Hali hiyo ilijidhihirisha Dar es Salaam jana wakati

umati mkubwa wa madaktari hao ulipojikusanya kwenye

mkutano wa hoteli moja jijini, na kutoa tamko la

kutorudi nyumba, huku wakisisitiza kuwa matokeo ya

mgomo wao yataanza kuonekana siku 12 zijazo na

kuendelea.

Wakati madaktari hao wakitangaza msimamo wao huo,

siku hiyo ya jana maofisa waandamizi wa Wizara ya

Afya na Ustawi wa Jamii wakiongozwa na waziri wao,

Dkt. Hadji Mponda, walikutana na waandishi wa

habari na kutoa majibu ya madai yao ambayo

hayaoneshi nuru ya kumaliza mgogoro unaoendelea,

bali kukuza ukubwa wa tatizo.

Pamoja na Dkt. Mponda kuwaambia waandishi wa habari

jana kuwa milango ya wizara yake ipo wazi tayari

kwa kukutana nao, madaktari hao nao  walijibu kuwa

mgomo unaendelea hadi pale watakapokutana na Waziri

Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, au ujumbe kutoka ofisini

kwake.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es

Salaam jana Mwenyekiti wa Jumuiya Mpya ya Madaktari

Dkt. Steven Ulimboka, alisema mgomo bado upo pale

pale na kwamba wao wanamtaka Waziri Mkuu Bw.

Pinda.

"Tunachosema ni kwamba milango iko wazi kwa

ajili ya mazungumzo na serikali, lakini serikali

iache kupotosha umma kwamba hakuna mgomo, ukweli ni

kwamba mgomo upo pale pale hadi kieleweke,"

alisema, Dkt. Ulimboka

Aliongeza kuwa hivi karibuni walikutana na uongozi

wa juu katika ofisi ya Waziri Pinda ambao ni Katibu

na Naibu Waziri, na kuzungumza nao kwa saa tatu,

lakini walishindwa kufikia muafaka, hatua

iliyosababisha mgomo kuanza.

"Serikali iache propaganda kwani kuna kamchezo kanachezwa, ndiko kanakowafanya wazunguke zunguke, hawana jibu moja la kutujibu, badala yake wanaitisha mikutano na

vyombo vya habari... kwanini wasije kuzungumza na

sisi ili muafaka upatikane?"Alihoji Dkt.

Ulimboka.

Alisisitiza kuwa; "Sisi tunachokifanya

tuko sahihi na wala hatujakosea, kama wao wanasema

tutafika mahali tushindwe hiyo si  kweli, ila

waache siku ziendelee kusogea mbele na ikifika siku

ya 12 na kuendelea majibu yatapatikana katika

hospitali zote nchini." 

Alisema madaktari watashangaa ikiwa watapata

taarifa kwamba Waziri Pinda anasafiri wakati

wananchi wanaendelea kufa hospitalini,  eti kwa

madai kuwa serikali imeshindwa kufikia muafa na

wao.

Wakati madaktari wakitoa msimamo huo, Dkt.

Mponda naye alikuwa na waandishi wa habari

akipangua kwa majibu hoja nane za msingi

zilizofikishwa na madaktari hao mezani kwake ili

zijadiliwe na hatimaye waweze kurejea kazini.

Alianza kwa kutoa mwito kwa madaktari ambao wapo

kwenye mgomo, kuacha mara moja ili kunusuru maisha

ya Watanzania wanaofika hospitalini kwa ajili ya

kupata tiba.

"Ni vyema madaktari wakatambua juhudi zinazofanywa

na serikali za kuboresha maslahi ya Sekta ya Afya

na wanatakiwa kuziunga mkono, hivyo basi tunawasihi

kurejea kazini", alisema Dkt. Mponda.

Katika hatua nyingine serikali imekiri mgomo huo kusambaa katika baadhi ya mikoa ingawa badohainataarifa ya athari zake.

Wakati huo huo waandishi wetu waliotembelea

baadhi ya hospitali mbalimbali jijini na  mikoani,

wameshuhudia baadhi ya ndungu wakifanya mipango ya

kuwahamishia wagonjwa wao hospitali za binafsi.

"Ndugu yangu hali ni mbaya, sielewi tunaenda wapi

hapa hospitali (Muhimbili) hakuna madaktari

tunaambiwa wapo kwenye mikutano wamegoma, ni bora

tuhamishe wagonjwa wetu tuwapeleke nyumbani,kwani

wengine hatuna kipato cha kuhamishia hospitali

binafsi," alisema.Mhudumu wa chumba cha kuhifadhi

maiti katika hospitali ya Muhimbili alipoulizwa

kama vifo vya wagonjwa vimeongezeka tangu mgomo huo

uanze, alijibu huku akitabasamu; "Hiyo siri ya

jeshi, lakini simama hapa mwenyewe uanze kuhesabu

zitakazoletwa.

"Mitaani nako walionekanakusikitika pale walipokuwa wakipitwa na magari ya wagonjwa (Ambulance) yakipiga ving'ora wakati wanakopelekwa kwa ajili ya matibabu ya juu zaidi madaktari wamegoma.

Wakati huo huo; taasisi inayojishughulisha na masuala ya afya na elimu kwa jamii nchini (SIKIKA) imeitaka  wizara hiyo kuchukua hatua za haraka kumaliza mgogoro huo, ili

kuepusha madhara makubwa yanayoendelea

kujitokeza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa jana

kwa vyombo vya habari na SIKIKA ilifafanua kuwa

wizara ina jukumu la kushirikiana na madaktari ili

kuboresha afya za wananchi.

"Ijulikane kuwa, jukumu la awali la wizara kwa kushirikiana na madaktari ni kuboresha afya za wananchi na kuokoa maisha yao, hivyo ni wajibu wao kufanya kazi kwa pamoja ili kufanikisha hili," ilisema taarifa na kuongeza.

Naye Mashaka Mhando,anaripoti Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Bw. Evarist Ndikilo, amesema

madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando mkoani

hapa, hawajaanza mgomo kama wenzao katika baadhi ya

mikoanchini, isipokuwa wanaweza kuungana nao

kuonesha mshikamano.

Hata hivyo alisema ofisi yake

imeongea nao kuona uwezekano wa kuepusha mgomo huo.

Akizungumza na Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii

iliyokuwa na ziara mkoani hapa, alisema madaktari

wa hospitali hiyo na zingine zilizopo mkaoni hapa,

wanaendelea na kazi na wala hawajagoma kama

wengine.

10 comments:

  1. Silikari iache kususuasua, iwalipe hao madakitari alaka sana. Figogo wa selikali finajilipa malupulupu menge pamoja na posho nyingi za mikutano isiyokuwa na ulazima wala tija. Alafu wabunge nao wanajiripa posho maradufu. Na wote hao wakiugua hata mafua wanakwenda kutibiwa majuu kwa pesa nyingi za waripa kod na walalahoi. Magari ya kifahali ya silikari makubwa ya pesa nying wana ela ya kununulia lakini hawana za kuongeza mishaala ya madakitari. Iyo ni akiri? Aiingia kichwani ata kidogo. Madakitali, waambie waripe kwanza ndo mtoe uduma.

    ReplyDelete
  2. Watanzania tufike mahali tumtambue adui yetu. Kwa kweli haingii akilini kuona wabunge wenye utitiri wa posho wakipandishiwa posho ambayo hata wao walishangaa, harafu serikali inashindwa kuongeza masilahi ya madaktari!. Hivi ni vipi mawaziri wa afya walishindwa kufika Don Bosco kuongea na madaktari kabla ya mgomo kuanza? wakati jana baada ya mgomo kuleta athari wakaweza kufika hapo starlight!!!!!!!!. Hawa viongozi hawatusaidii ila wapo kwa masilahi yao binafsi.

    ReplyDelete
  3. unajua taaluma ni ki2 muhimu cna maishani mwa binadamu na unaweza mtu ukafanya kazi sehemu yeyote ile dunian bila bugudha ya mtu wa wala wanaohitaji huduma yako bali kwa sisi serikali yetu sio wazalendo kwan nan na ana nguvu gani kwa kazi ipi na alipwe mshahara mnono mbunge bila kuwa na kazi muhim katika jamii au huyo jaji mkuu au majaji wenzake wanakazi ipi muhimu katika kuokoa maisha ya watanzania moja kwa moja,tazama mara mbili naunga mkono moja kwa moja mgomo wa madakitari,solidarity forever

    ReplyDelete
  4. hivi hawa mawaziri pamoja na rais wao wanpepo gani ambao wanahitaji waombewe ndio hawatoke ona kiranja wao mkuu kaenda kuuzulia mkutano wa nchi 20 tajiri ikiwa sis ni top ten ya mwisho na kwa kutumia takribani 300millions za walipa kodi wengi wao ni maskini na tunaishi chini ya dora moja this is not true then lets put all a side and pray for a god to save us,naomba mdingatie taaluma za watu ambao wameangaika darasi kwa muda mrefu arafu leo umunyonye noooo,tukiwa chuo/shule tunavumilia vya kutosha na huku nako

    ReplyDelete
  5. CHONDE CHONDE PINDA KAMA KWELI UNAFANYA KAZI FUKUZA MAWAZIRI WAZEMBE NA WATENDAJI WOTE WA SERIKALI,ULISEMA HATA POSHO ZA WABUNGE NI NDOGO:
    MADAKTARI ENDELENI NA MGOMO KWA HAO WANAOWAFUKUZA WANATIBIWA INDIA HAWANA SHIDA ETI.
    PINDA TANZANIA YA LEO SIYO ILE YA ZAMANI ETI
    KUFUKUZANA SIYO JAWABU LA KUTIBU WAGONJWA,TANZANI TUNASHIDA YA MADAKTARI, LAZIMA TUJIULIZE KWANINI WANAGOMA?

    ReplyDelete
  6. Mh. Pinda mbona unatumia mabavu wakati swala la madaktari linajulikana? Hapa sio mahala pa kutumia nguvu kwani madaktari wa interns walifukuzwa ndio balaa likaanza na wewe unamwagia moto petroli, kaa na hao madaktari mujadili kwa kina jinsi ya kuwatatulia matatizo yao ukimalizana nao lazima watarudi kazini... Shida yao ni kusikilizwa na yale ya muhimu yatimizwe acheni utemi damu itamwagika na sisi wananchi wa kawaida ndio tutapata shida... Mungu awaongoze katika kutoa maamuzi..

    ReplyDelete
  7. Kama ziko za kuwalipa posho wabunge kwanini wasiwalipe madaktari na wauguzi? Haiingii akilini kuona viongozi wetu wanafanya ukatili na uonevu wa aina hii. Madaktari na wauguzi msimamo wao uwe pale pale. Viongozi wasidhanie wanaweza kuwatisha. Ni lini hawa wenda wazimu watakuwa sober na kusikiliza vilio vya wananchi na wanataaluma?

    ReplyDelete
  8. Hivi wanaharakati wa haki za binadamu mnatushaurije sisi wananchi? Tunaweza kuishitaki serikali kwa uzembe na kutowajibika kulikosababisha vifo na hasara za kibinadamu kutokana na matatizo haya? Tupeni ushauri jamani. Tuishitaki serikali itulipe fidia. Washike adabu kufanya dharau na ujeuri kwa maisha ya watu. Lazima hii serikali dhalimu iwajibishwe.

    ReplyDelete
  9. Hivi wanataka kutuambia hakuna pesa za kulipa madakatari haki zao,pesa zinaishia tu kwenye mambo ya siasa,ushabiki wa siasa.majuzi wamemaliza mabilion kwa ajili ya miaka 50 ya uhuru,mabilioni ya changuzi ndogo igunga,pesa za rada zikarudishwa zimeenda wapi mbona yalikuwa mabilioni.madaktari walipwe,walimu walipwe,na wote wenye madai sugu,serikali wanajinufaisha wenyewe mkomae.wao wanatibiwa india,na regency,agakhan hindmandal.wanasababisha vifo kwa umafia wao.pesa zipo,zitoke.ngoja watangaze uchanguzi wa majimbo yaliyowazi,wataona reaction za walala hoi.haiwezekani wanakaa tu kimya.huko bungeni wamefuata posho wala si kujadili.wanaacha watu wanakufa wanaenda kujadil miradi ya nani na watu wenyewe wanakufa?

    ReplyDelete