NEW York Marekani
MCHEZAJI nyota wa mpira wa kikapu, Kobe Bryant na mkewe Vanessa wako mbioni kutengana.
Hiyo imetokana na baada ya kutambulika kuwa Kobe tayari amefanya taratibu kuandikisha nyumba mbili kwa jina la mkewe ambaye atatengana naye siku zijazo.
Mtandao unaooandika habari za wasanii nyota Hollywood, umefanya uchunguzi na kugundua kuwa Januari 5, Kobe aliachia nyumba mbili kwa Vanessa na pia katika siku hiyo Vanessa aliamua kuiachia nyumba ya tatu kwa Kobe.
Chanzo kimesema kuwa sasa Vanessa ni mmiliki wa nyumba ambayo alikuwa akiishi na Kobe iliyo Newport Coast huku nyumba ya pili ambayo ataimilimili jumla ni ya karibu ambayo alikuwa akiishi mama yake.
Awali mtanda wa TMZ uliandika stori Desemba 16 kuwa Vanessa amefungua mashitaka akidai talaka kutoka kwa Kobe.
Ingawa kulikuwa na habari kuhusu kuwepo hali ya kumaliza tofauti zao, lakini hali ya kugawana mali iliyoaonekana imeonesha kuwa talaka iko karibuni kati yao.
Mwakilishi wa Kobe, Michael Sitrick, alisema kuwa hana cha kueleza kuhusu jambo hilo.
No comments:
Post a Comment