16 January 2012

Nando atajwa kikosi cha Angola

LUANDA,Angola

MCHEZAJI Nando Rafael ameitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya  Angola kwa ajili ya fainali za Mataifa ya Afrika, lakini huenda hasicheze kwenye fainali hizo za mwezi huu zitakazofanyika katika nchi za Guinea ya Ikweta na  Gabon.

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), pamoja na mchezaji huyo kutajwa kwenye kikosi hicho lakini Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) bado halijatoa kibali kwa mchezaji huyo kuichezea Angola.

BBC ilieleza kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka  28 tayari alishaichezea timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 21 ya Ujerumani, hivyo anahitaji kibali maalumu kutoka FIFA.

Hata hivyo FIFA ilisema hadi jana, ilikuwa haijapokea maombi yoyote ya Angola ya kumtumia Rafael katika michunao hiyo.

Kikosi cha Angola, kilichotaja majina yake Jumamosi, kilitakiwa kuwasilishwa CAF katikati ya wiki iliyopita.

Katika kikosi hicho, Kocha Lito Vidigal, amemuita beki  Kali na washambuliaji Flavio  na Love, ambao wamewahi kuichezea Angola kwenye fainali tatu zilizopita.

Angola, ambayo mwishoni mwa wiki ilikuwa ikicheza mechi yake ya mwisho ya kujiandaa na michuano hiyo dhidi ya timu ya  Sierra Leone,mjini  Cabinda,imepangwa Kundi  B ambapo itakutana na timu za Taifa za Burkina Faso, Ivory Coast na  Sudan.

Kikosi kamili kilichotangazwa na kocha huyo ni kama ifuatavyo,walinda mlango ni Carlos, Hugo (Kabuscorp), Wilson (Primeiro Agosto).

Mabeki  Amaro, Dani Massunguna na  Kali (wote Primeiro Agosto), Marco Airosa (AEL Limassol, Cyprus), Mingo Bille (Primeiro Agosto), Zuela (Atromitos, Ugiriki)

Viungo Andre Makanga (Al Jahra, Kuwait), Dede (AEL Limassol, Cyprus), Gilberto (Lierse, Ubelgji), Mabina, Miguel (wote Petro Atletico), Osorio (Recreativo Caala), Xara (Petro Atletico)

Washambuliaji ni Djalma (FC Porto, Ureno), Flavio (Lierse, Ubelgji), Jose Pierre Vunguidica (Preussen Munster, Ujerumani), Love (Petro Atletico), Manucho (Real Valladolid,Hispania), Mateus Galiano (Nacional, Ureno), Nando Rafael (FC Augsburg,Ujerumani).

No comments:

Post a Comment