26 January 2012

MAHAKAMA KUU KUANZA KUSIKILIZA KESI YA ALIYEKUA MGOMBEA URAIS WA BURUNDI.

Na Grace Ndossa

MAHAKAMA Kuu kanda ya Dar es Salaam  itaanza kusikiliza kesi ya kumshikilia  aliyekuwa mgombea urais nchini Burundi Bw. Alex Sinduhije Febuari 6 mwaka huu.

Uamuzi huo ulitolewa jana  mahakamani hapo na jaji Laurence  Kaduri baada ya  mawakili wakuu wa serikali Bw. Obed  Kameya na Bw. Edwin Kakolaki walipofika mahakamani kwa ajili ya kuwakilisha mkuu wa  jeshi la polisi (IGP) Ofisi ya mwanasheria Mkuu
wa serikali.

Wakili wa serikali  Bw.Obed Kameya  aliieleza mahakama kuwa walipata  amri ya kuitwa mahakamani jana mchana, hivyo wanaomba wapewe muda  wa siku saba ili waweze kujibu madai hayo.

Jaji Kaduri alikubalina na ombi hilo na kutoa muda wa siku saba  wawe wamejibu kwa njia ya maandishi hadi 31 januari wawe wameshajibu.

Hata hivyo wakili anayemtetea  Bw. Senduhiji Bw. Hurbet Nyange  atatoa majibu ya nyongeza  februari 3 mwaka huu.

Bw. Sinduhiji alikamtwa katika uwanja wa ndege wa Kimatifa wa Mwalimu Julias Nyerere kwa hati ya shirika la polisi la kimataifa la (Interpol)akitokea Uganda kluja Nchini na Januria 13 alifikishwa mahakamani kisutu lakini hakusomewa mashtaka.

Mtuhumiwa huyo  alikamatwa na polisi  na kushikiliwa na polisi kwa siku mbili mfululizo katika kituo cha polisi kati Dar es Salaam huku kukiwa hakuna maelezo yoyote kutoka serikalini na  jeshi hilo kuhususababu za kukamtwa kwake.

Wakati akikamatwa na Interpol Bw. Sinduhiji  alituhumiwa na serikali ya burundi kuhusika na mauaji ya mwakili wa shirika la afya la umoja  wa Mataifa(WHO)Dkt KassiManlan raia wa Ivory coast na aliyekuwa mtumishi wake na pia mauaji ya halaiki ya  katumba.


No comments:

Post a Comment