02 October 2013

SAKATA LA YANGA SC, PAPIC LAFIKIA PATAMU



Na Fatuma Rashid
   Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), limewasilisha rasmi suala la madai ya aliyekuwa Kocha wa Yanga, Kostadin Papic dhidi ya klabu hiyo katika Kamati ya Hadhi ya Wachezaji.

 Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Ofisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema FIFA imepeleka rasmi suala hilo katika kamati yake hiyo, baada ya kupokea vielelezo vya Papic anayedai kuidai Yanga dola 10,000 za Marekani pamoja na vile vya Yanga inayodai kumlipa kocha huyo fedha zote alizokuwa akiidai klabu hiyo.
   Wambura alisema kwa taratibu za FIFA, hivi sasa haitapokea vielelezo vingine kutoka pande hizo mbili na badala yake, Kamati hiyo inayoongozwa na Theo Zwanziger, kutoka Ujerumani itafanya uamuzi na kuziarifu pande husika. Zwanziger kitaaluma ni mwanasheria.
  Aliongeza kuwa Papic, aliyeinoa Yanga kwa vipindi viwili tofauti aliwasilisha malalamiko yake FIFA akidai hadi mkataba wake unamalizika klabu hiyo, ilikuwa haijamlipa dola 10,000 za Marekani.
  Katika sakata hilo, uongozi wa Yanga uliwahi kuulizwa kuhusu madai hayo ambapo walisema hadai chochote, huku wakiongeza kwamba kocha huyo alikuwa analipwa kila baada ya miezi mitatu na walionesha hati zote za malipo waliyokuwa wakimlipa

No comments:

Post a Comment