- MWALIMU ALIYEMBAKA MWANAFUNZI 'MTEGONI'
- MAHAKAMA YAMPELEKA GEREZANI MIAKA 30
Na Nickson
Mahundi, Ludewa
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ludewa, mkoani
Njombe, imemhukumu kifungo cha miaka 30 gerezani na kuchapwa viboko 30 mwalimu
wa Shuile ya Msingi Ingwachanya.
Mwalimu
huyo, Bw. Romanus Msango, mkazi wa Lupembe, wilayani Njombe, alitiwa hatiani
kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa miaka 14 (jina linahifadhiwa) na kumuumiza
vibaya sehemu za siri.
Akisoma
hukumu hiyo Septemba 6 mwaka huu, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya
ya Ludewa, Bw.
Fredrick
Lukuna, alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa
mashtaka ambao haukuwa na shaka yoyote.
Alisema
mshtakiwa alitenda kosa hilo
kinyume na kifungu namba 1309(1) na 31(1) cha kanuni ya adhabu ya mwaka 2002
hivyo adhabu hiyo ni fundisho kwa wengine.
"Natoa
adhabu hii ili kukomesha vitendo hivi kwenye jamii
kwani
vinaleta madhara makubwa kwa watoto na wanawake pamoja na kusababisha magonjwa
ya kuambukiza," alisema.
Awali ilidaiwa na Mwendesha Mashtaka, Edison Kasekwa kuwa,
mshtakiwa alitenda ukatili huo wa kinyama Agosti 20,2012 katika Kijiji cha
Masimbwe, Kata ya Mlangali.
Alisema kabla
mshtakiwa hajatenda kosa hilo,
alimshambulia mwanafunzi huyo, kumbaka na kumlawiti jambo ambalo lilimsababishia
maumivu makali.
"Serikali ilimpa mshtakiwa dhamana
kubwa ya kulea watoto ambao ni nguvukazi ya Taifa la kesho lakini amewageuka na
kutenda kitendo ambacho ni kinyume na maadili ya kazi yake, kuidharirisha
taaluma hivyo naomba mahakama itoe adhabu kali iwe fundisho kwa walimu
wengine," alisema.
Bw. Kasekwa aliongeza kuwa, mshtakiwa
alikusudia kutenda makosa hayo kwa sababu alimfuata mwanafunzi huyo shambani
wakati akivuna mahindi na wenzake ambao walikimbia kwenda kijijini kutoa
taarifa baada ya mshtakiwa kumkamata mwenzao na kumpeleka kichakani.
Wa k a t i h u o h u o , wa
t u wawili Bahati Mtega na Flowin Mtweve, wote wakazi wa Milo,
wamehukumiwa kifungo cha maisha gerezani na kuchapwa viboko 12 kila mmoja kwa
kosa la kumbaka mke wa mtu na kumsababishia maumivu makali
Mwalimu kupewa dhamana ya kulea watoto kielimu na kisha kuwageuka ni kwaida kwa TZ KTK fani zingine.
ReplyDeleteMara ngapi tumeona manesi wakinyanyasa wagonjwa? Mara ngapi viongozi wakipewa dhamana ya kulindamali ya umma wanaifisadi?
Ni mara ngapi viomgozi wa dini tena hao ndo kabisa.Mie nimeshuhudia sista mmoja kijijini kwetu akimsingizia mama yake kuwa ni mchawi, na kumpa pesa za kutosha mdogo wake ili amnyanyase mama yao kwa kusudio la kuharakisha kifo chake kwa manyanyaso.
Kwa hiyo bunge letu liache mapigano , badal yake liangalie upya sheria za kulinda wananchi wake kikatiba
watu wa mwogope Mungu,watoto wetu tuwafiche wapi? Watanzani? hata wazee ,viongozi wa serikali,dini wafanya biashara ngono imekuwa ni km pombe kwao,watoto wa kike hawajiamini ,hata ktk kazi kwa mapokeo mabaya wanayo ya ona kwa walimu,lecture,profesor ,huwezi kuona mwanamke anasumbuliwa Amerika km nyumbani watu wote wako chini ya sheria,nchi yenye kila kitu lakini hata utamaduni wetu tunashidwa kuuenzi Mungu tusaidie.
ReplyDeletevitendo vya ubakaji nchi hii vinatisha sana hii ni kutokana na kukosa maadili. je mtoto wake wa kumzaa angelifanyiwa hivi angejisikaje? watu wenye tabia kama hii wanastahili kufungwa maisha kwani ameharibu maisha ya huyo mtoto na hicho kitendo kitamuathiri huyo mtoto katika maisha yake yote.
ReplyDelete