Na Hussein Makame, Maelezo
TUME ya Vyuo
Vikuu Tanzania (TCU) imekataa majina ya wanafunzi 8,805 walioomba kujiunga na
masomo ya shahada ya kwanza katika taasisi za elimu ya juu nchini kwa mwaka wa
masomo 2013/2014 kutokana na sababu mbalimbali zilizojitokeza kwenye fomu za
waombaji.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Sifuni Mchome, wanafunzi
hao hawakuchaguliwa na tume hiyo kujiunga na vyuo vikuu kutokana na maombi yao
ya programu zote walizochagua kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa.
Taarifa hiyo
ilieleza kuwa sababu za kutochaguliwa kwa wanafunzi hao ni pamoja na ushindani
wa wanafunzi katika programu walizochagua, wanafunzi kushindwa kuwasilisha
programu walizochagua na kuchagua programu ambazo hawana sifa nazo.
Hata hivyo, TCU
imesema inawapa nafasi nyingine wanafunzi hao kuomba tena kwa awamu ya pili kwa
kuchagua programu nyingine ambazo wana sifa nazo kupitia mfumo wa udahili wa
TCU, ambao umeshafunguliwa tangu Julai 29 hadi Agosti 9, mwaka huu,
utakapofungwa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwanafunzi
anatakiwa kuangalia jina lake katika orodha ya wanafunzi ambao hawakuchaguliwa
na TCU, orodha inayopatikana kwenye tovuti ya taasisi hiyo.
"Ba a d a y a mwa n a f u n z i
kuthibitisha jina lake kwenye orodha ya wanafunzi ambao hawakuchaguliwa iliyoko
kwenye tovuti ya TCU, unatakiwa kufuata masharti yafuatayo, chagua programu
moja tu kutoka kwenye orodha ya programu inayopatikana kwenye tovuti ya
TCU," ilisisitiza taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa masharti hayo, pia mwanafunzi
anatakiwa kufungua mwongozo wa udahili unaopatikana kwenye tovuti hiyo na
kuthibitisha kwamba anayo sifa stahiki ya kujiunga na programu aliyoichagua.
umakini unahitajika wakati wa kuomba vyuo, si kila credits za masomo zinafit kuomba course yoyote vyuoni. huwezi kuwa na pass za HGL then ukaomba medicine eti kwa sababu kuna fursa ya kuomba kozi zaidi ya moja.
ReplyDelete