30 August 2013

TRA YAANZA KUTUMIA MFUMO MPYA BANDARI



Na Ester Maongezi
MAMLAKA ya Mapato Ta n z a n i a ( T R A ) imesema kuanzia sasa itakuwa inapokea taarifa moja kwa moja kutoka Mamlaka ya Bandari Tanzania juu ya mizigo inayoingia na kutoka ili kuondoa tatizo la udanganyifu uliokuwa ukifanywa na wafanyabiashara na watendaji. Hatua hiyo inalenga ukwepaji ulipaji kodi

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Ofisa Elimu Idara ya Kodi wa TRA, Richard Kayombo, wakati akizungumza na waandishi wa gazeti hili. Alisema kwa kipindi cha nyuma taarifa zilikuwa zinaenda bandarini kwanza na wao kupewa taarifa tu mzigo unapotoka jambo ambalo lilikuwa likiwapa shida wakati wa ufuatiliaji na ukaguzi.
Kayombo alisema ilikuwa ikiwapa shida kwasababu ya kutokushirikishwa katika kipindi cha mizigo inapoingia bandarini kitu ambacho kilichangia sana wao kutokupata taarifa sahihi. "Kwa sasa TRA tunapata taarifa mapema kabla ya mzigo kushushwa kitu amabcho kinatusaidia kujua kontena linakuwa na mzigo wa aina gani na wenye thamani ya kiasi gani," alisema Kayombo.
Katika hatua ya kuboresha m a p a t o , TRA i m e z i n d u a mfumo mpaya wa udhibiti wa bidhaa katika bandari ya Dar es Salaam ujulikanao kama Cargo Management System ili kuboresha na kurahisisha uondoshaji wa bidhaa banadarini na ubadilishanaji habari kati ya watendaji.
Kayombo alisema anaamini mfumo huu mpya ulioanza tangu Agosti 14, utasaidia kuweka rekodi za bidhaa zinazoingia nchini na unaziwezesha mamlaka hizo kufuatilia taarifa kwa ufanisi zaidi, pia kuzuia wizi wa bidhaa kutoka bandarini.
Aliongeza kuwa mfumo huo utawawezesha mawakala wa meli kutuma taarifa ya bidhaa kwa idara ya Forodha wakiwa mahali popote penye mtandao, pia utasaidia kulinda ushuru na kodi za Serikali na mali za wateja kwa ufanisi zaidi.
Kayombo alitoa mwito kwa wadu wengine kutoa ushirikiano na kuimarisha mifumo yao ili iwe rahisi kubadilishana taarifa na idara ya Forodha huku akisema kuwa endapo kutakuwa na hitilafu zozote basi wananchi wasisite kuwasiliana na TRA.

No comments:

Post a Comment