30 August 2013

MAOMBI YA RUFAA DHIDI YA ZOMBE WIKI IJAYO



 Na Rachel Balama
WAPINGA rufaa katika k e s i y a ma u a j i y a w a f a n y a b i a s h a r a iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na askari wenzake wanane walioachiwa huru katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini wameiomba Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kupewa muda ili kuwasilisha majibu ya maombi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) ya kuongezewa muda wa kukata rufaa.

Akiwasilisha maombi hayo mbele ya Jaji Aloyisius Mujuluzi, wakili wa wapinga rufaa Majura Magafu, aliiomba wapewe muda ili waweze kuwasilisha majibu dhidi ya DPP. Alisema kuwa walichelewa kupata maombi ya DPP dhidi ya wateja wao kwa kuwa maombi hayo yalitumwa moja kwa moja kwa wateja wao.
"Mheshimiwa Jaji, tunaaomba muda wa kuwasilisha majibu yetu kwa kuwa, upande wa Serikali uliwatumia moja kwa moja wateja wetu ndipo wateja hao walitutumia sisi," alisema Magafu.
Mbali na Magafu wapinga rufaa hao pia wanatetewa na mawakili Richard Rweyongeza na Dennis Msafiri.
Akijibu hoja hiyo wakili upande wa Serikali, Timoth Vitalis, alisema kuwa hawana pingamizi na hoja hiyo. Hata hivyo Jaji anayesikiliza rufaa hiyo, aliutaka upande wa wapinga rufaa kuwasilisha majibu yao Septemba 2, mwaka huu ambapo na upande wa serikali uwasilishe majibu Septemba 4, mwaka huu.
Jaji aliahirisha shauri hilo hadi Septemba 5, mwaka huu ambapo mahakama itaanza kisikiliza. DPP aliwasilisha maombi mahakamani ya kuongezewa muda wa kukata rufaa, baada ya mahakama ya Rufaa ya Tanzania kutupilia mbali rufaa ya awali kwa sababu ilikuwa na makosa kisheria. Rufaa hiyo ilitupwa baada ya kubaini kuwapo kwa dosari katika hati ya kusudio la kukata rufaa na mahakama kukataa kuamuru makosa yaliyojitokeza yafanyiwe marekebisho.
Katika shauri hilo mbali na Zombe wajibu rufaa wengine ni askari Christopher Bageni, Ahmed Makele, Jane Andrew, Koplo Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abeneth Saro, Rajabu Bakari na Festus Gwasab.
Serikali ilikata rufaa hiyo kupinga hukumu iliyotolewa Agosti, 17, mwaka 2008 na Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam iliyowaachia huru.

No comments:

Post a Comment