12 August 2013

CHAKULA CHAUA NDUGU WANNE,13 HOI



Cresensia Kapinga
WATU wanne wa familia moja wamefariki na wengine 13 wamelazwa hospitalini kutokana na kula chakula chenye sumu wakati wa sikukuu ya Idi el Fitri.Watu hao wamelazwa Kituo cha Afya cha Lusewa wilayani Namtumbo na Hospitali ya Serikali ya Mkoa wa Ruvuma (HOMSO).

Kamanda wa Polisi Mkoa Deusidebit Nsimeki, alisema tukio hilo lilitokea Agosti 9, mwaka huu saa 7:00. Kamanda Nsimeki, alisema siku hiyo kabla ya tukio, Salum Mumba, alinunua samaki aliyepeleka nyumbani kwa ajili ya sikukuu ya Idi.Kamanda Nsimeki alisema k a t i k a t u k i o h i l o P o l i s i wanamshikilia mtu mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina ambaye atasaidia polisi kwenye upelelezi wake.
Alisema baada ya kula chakula hicho, haikuchukua muda mrefu mtoto alianza kuumwa naye baadaye alifariki dunia. Baadaye watoto wawili walianza kuumwa na kufariki. Watu wengine 13 walianza kuumwa baadaye majirani walipata taarifa kuwakimbiza watu hao hospitali.
Aliwataja waliolazwa katika kituo cha afya cha Lusewa kuwa ni Tazamio Mumba, Zidani Mumba, Ramadhani Mumba na Zahara Mumba wote wakazi wa kitongoji Tulieni B.
Waliolazwa katika hospitali ya Mkoa wa Songea kuwa ni Gairi Mumba, Zamoni Mumba, Fatuma Rashidi, Samidu Mumba, Asha Omary na Sharifa Mumba.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi ya Hospitali ya Mkoa Songea Dkt. Benedictor Ngaiza alisema wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo hali zao zinaendelea vizuri.

No comments:

Post a Comment