19 July 2013

CHADEMA YAJA NA MKAKATI MPYA


Na Goodluck Hongo

CHAMA cha Demokrasia na Ma e n d e l e o ( CHADEMA) kimepanga kuzunguka nchi nzima kwa usafiri wa anga, majini na nchi kavu, kufanya mikutano ya hadhara ambayo itakuwa ni mabaraza yake ya katiba ili kuwapa fursa wananchi kujadili rasimu ya katiba mpya na kutoa maoni yao.Akizungumza juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Stendi ya Malori, Majengo, mjini Songea mkoani Ru v uma , Mwe n y e k i t i wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema utaratibu mzima wa namna mabaraza ya katiba ya chama hicho yatakavyoendeshwa kwa nia ya wananchi kutoa maoni yao na namna ya kuboresha rasimu ya katiba mpya, utatolewa hivi karibuni.
Alisisitiza kuwa wanataka katiba mpya inayotokana na mwafaka wa Watanzania wote.Alisema tangu chama hicho kianzishe ajenda ya katiba mpya, kimekuwa na dhamira ya kuona Watanzania wakijipatia katiba inayotokana na matakwa yao kwa ajili ya kusimamia na kulinda masilahi yao."Ndugu zangu, Watanzania wenzangu wa Songea, mtakumbuka kuwa ajenda hii ya katiba ilikuwa ni ajenda ya CHADEMA, na tuliisimamia kwa miguu yote, mnajua hilo na haikuwa agenda wala haijawahi kuwa ajenda ya CCM, ndiyo maana sasa chama hicho kinafanya juhudi za kupingana na maoni ya Watanzania katika masuala ya msingi yaliyomo ndani ya rasimu.

Alisema hadi sasa tayari mabaraza ya katiba yameanza kukutana, lakini asilimia kubwa yametawaliwa na CCM, lakini wao pia na Watanzania wengine wote wanaoipenda nchi yao, wana fursa ya kuunda mabaraza yao."Tutakuwa na mabaraza ya katiba nchi nzima, ambayo tutayafanya kwenye mikutano ya wazi ya hadhara. Hatutajifungia ndani kama wanavyofanya wao," alisema.Mbowe aliongeza kusema kuwa katika rasimu ya katiba mpya pamoja na kuwepo kwa masuala mengi, kuna mambo manne ambayo Mtanzania yeyote makini na anayeipenda nchi yake atalazimika kukubaliana na mapendekezo ya Tume ya Jaji Joseph Warioba.

"Sasa jiandaeni kwa mabaraza ya katiba ya CHADEMA, tutazunguka nchi hii ikibidi kwa ndege, yatakuwa yakifanyika kwenye sehemu za wazi, ambayo siku nzima wananchi wa eneo husika watajadili rasimu ya katiba mpya wakitoa maoni yao, kisha tutayachukua pamoja na saini zao...nchi nzima tutafanya, viongozi wote, wabunge wote watasambaa nchi nzima," alisema Mbowe.Al i b a i n i s h a k uwa y e y e h a t amu o g o p a r a i s , l a k i n i atamheshimu, hataogopa polisi lakini atawaheshimu, hataogopa jeshi lakini ataliheshimu jeshi na hatamheshimu mtu yeyote asiye heshimu ubinadamu au mtu mwingine.Alisema uchaguzi wa kata nne mkoani Arusha wameshinda kwa mapambano ya damu ambapo watu wao walipigwa kila mahali na kukatwa mapanga na mashoka na vijana wa CCM.

No comments:

Post a Comment