21 December 2012
SSRA yatoa mafunzo kwa wadau wa mifuko
Na Heri Shaaban
MAMLAKA ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Tanzania (SSRA)imetoa mafunzo kwa wadau wa mifuko kuhusiana na miongozo ya namna ya kujisajili wanachama katika mifuko ya jamii
Mafunzo hayo yalifanyika Dar es Salaam jana,na kushirikisha wafanyakazi wa mamlaka na wadau kutoka vyama mbalimbali vya wafanyakazi
Akizungumza katika mafunzo hayo Mkurugenzi wa Sheria wa SSRA Ngabo Ibrahimu alisema kuwa madhumuni ya mafunzo hayo kuwataka wanachama wapya wachague mifuko gani ya kujiunga.
Pia wajili wasiwalazimishe wafanyakazi katika mifuko waipendayo kwa maslai yao binasfi kwani jukumu la kujiunga analo mfanyakazi mwenyewe.
"SSRA imetoa mafunzo yenye lengo la kuwapanua wafanyakazi kielimu ili wasipelekeshwe na wajiri wao wakawapangia mifuko ya hifadhi ya jamii ya kujiunga wakati sio jukumu la mwajili"alisema Ibrahimu.
Aliwataka wafanyakazi wawe huru kwa kuangalia maslai yao wasibughuziwe na wajiri wao kwani jukumu la kujiunga katika mifuko ya hifadhi ya jamii analo mfanyakazi sio mwajiri.
Pia aliwataka wajili watoe fursa katika mifuko yote ili wafanyakazi wachague mifuko waipendayo kwa maslai yao wenyewe.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wafanyakazi (TUICO)Bw.Jones Majura walipendekeza wafanyakazi wanapoachishwa kazi wawe na malipo yatakayoweza kumpatia fedha za kula na familia kabla kupata kibarua kingine.
.
Mapendekezo hayo walipendekeza kufuatia wafanyakazi wengi baada mikataba yao ya kazi kumalizika wanasota nyumbani bila kibarua wala mshahara huku familia zikiwategemea.
Walipongeza SSRA kwa utoaji wa mafunzo hayo kwa ajili ya utoaji wa elimu hiyo iweze kutumiwa na wafanyakazi wote nchini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment