20 July 2012

Mtibwa Sugar kumtangaza kocha karibuni


Na Mwali Ibrahim

TIMU ya soka ya Mtibwa Sugar, inatarajia kumtangaza rasmi hivi karibu Kocha atakayekinoa kikosi hicho kwa ajili ya Ligi Kuu.

Mtibwa ambayo imeingia kambini Julai 15 mwaka huu kwa ajili ya maandalizi ya ligi hiyo kwa sasa inanolewa na kocha msaidizi, Patrick Mwangata.

Akizungumza kwa simu Mwenyekiti wa Mtibwa Sugar, Jamal Baiser alisema timu hiyo imeanza mazoezi mapema ili kujiweka sawa na ligi msimu ujao chini Mwangata, wakati wakimsubiri Kocha mpya.

"Tunatarajia kumtangaza kocha wetu mpya ambaye atakinoa kikosi chetu kwa ajili ya Ligi Kuu ingawa kwa sasa ni mapema mno kumtaja hadi tutakapokamilisha mipango yetu yote," alisema.

Akizungumzia kuhusu kuanza maandalizi mapema, alisema wamefanya hivyo kwa kuwa anatarajia ligi ya mwaka huu itakuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kujiandaa kikamilifu.

"Siku zote kwenye ligi kila timu inaonekana kujiandaa mapema, sisi tumeamua kuanza mapema zaidi ili kuwaweka fiti wachezaji wetu," alisema.

No comments:

Post a Comment