16 May 2012
Wauguzi Ilala kuanzisha SACCOS
Na Heri Shaaban
WAUGUZI wa Manispaa ya Ilala wameanzisha Chama cha Kuweka na Kukopa SACCOS yenye wanachama 76 kwa ajili ya kuweka amana zao.
Akizungumza na Majira hivi karibuni Ofisa Muuguzi wa Afya ya Jamii Bi.Beauty Obadia aliwataka wauguzi waliopo ndani ya manispaa hiyo kujiunga katika chama hicho waweze kuweka hisa zao.
Bi.Obadia alisema kuwa chama chao kina wanachama hai 76 na kiwango cha hisa zilizokusanywa zaidi ya milioni 6.
"Fedha hizi tumekusanya kwa kiwango cha hisa 20 kila mwana chama aliyejiunga katika chama hichi ,"alisema Bi.Obadia.
Aliwaomba watumishi wa manispaa hiyo wajiunge katika benki hiyo ili waweze kujiendeleza kwa kuweka na kuchukua mikopo kwa ajili ya shughuli mbalimbali.
Alisema kuwa toka benki hiyo ianzishwe wauguzi wa Ilala imewakomboa kwa kuwainua kiuchumi kutokana na kuchukua mikopo bila riba
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment