18 May 2012

Ukaguzi vyombo vya baharini utapunguza ajali nchini



Na Tumaini Maduhu

SEKTA ya usafirishaji  ni moja ya kiunganishi cha maendeleo nchini kutokana na umuhimu wake wa kuunganisha sehemu moja na nyingine.

Sera ya Taifa ya Usafiri ya mwaka 2003 ambayo sasa inafanyiwa maboresho ili iende sambamba na mpango mpya wa serikali wa miaka mitano, yaani 2012/2017 itazingatia maendeleo na teknolojia mpya ijitokeze katika uendeshaji wa sekta ya usafiri wa anga kitaifa na kimatifa.

Sekta hii imekuwa, ikiwakomboa watu kwa kufanikisha majukumu yao kwa kuwarahisishia kubalishana bidhaa mbalimbali na kuwatoa watu sehemu moja kwenda nyingine.

Ni ukweli usiopingika kuwa, nchi yeyote Duniani bila kuwa na usafiri ni sawa usiku wa giza ambao haujui ni lini utapata mwanga wakuangaza.

Hali hii imejidhihirisha, kutokana na watu wengi kukwama katika majukumu yao kutokana na kukosa usafiri.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu Sumatra Bw. Ahmad Kilima anasema, mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Shirika la la usafiri wa baharini Duniani(IMO) wameamdaa warsha  kwa wasafirishaji wa baharini ili kuwajengea ujuzi na weledi wa kudhibiti ajali za baharini.

Anasema kuwa, warsha hiyo imeshirikisha mabaharia, wamiliki wa vyombo vya usafirishaji baharini, chuo cha usafirishaji (DMI).

"Tunaamini mafunzo, haya yatawajengea ujuzi na weledi ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali baharini pamoja na namna ya kukagua vyombo vyao kabla ya kusafirisha abiria," anasema Bw Kilima.

Anasema kuwa, kupitia warsha hiyo wanaamini ajali zitapungua baharini kutokana na wadau kutoka sekta mbalimbali za usafirishaji na Wizara husika kutoa mchango wao namna ya kudhibiti ajali za baharini.

Bw.Kilima anasema kuwa, katika kuhakikisha ajali za baharini zinapungua mamlaka hiyo inajitahidi kukagua vyombo vya usafirishaji kabla ya kutoa leseni ili kudhibiti ajali za baharini.

Anasema kuwa, njia nyingine inayotumiwa na mamlaka hiyo katika kuhakikisha wanadhibiti ajali za baharini ni kuvifungia baadhi ya vyombo vinavyosababisha ajali kwa uzembe na kupoteza maisha ya watu.

"Tumeamua kutoa, adhabu hii ikiwa ni moja ya mpango mkakati wetu wa kuhakikisha tunadhibiti ajali zinazosababishwa  na madereva wazembe," anasema, Bw Kilima.

Anatoa mwito kwa vijana kusomea taaluma ya ubaharia ili wapatikane wataalamu wenye mwamko  na wenye tija katika kudhibiti ajali za baharini.

Anasema kuwa, vijana wengi wakiwa na mwamko wa kusomea fani ya ubaharia kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali zisizokuwa za lazima.

Hata hivyo anasema kuwa, mamlaka hiyo imekuwa ikikikaa na wamiliki wa vyombo vya usafiri mara kwa mara ili kujengeana ujuzi na uzoefu wa kudhibiti ajali za baharini.

"Tunaamini tukishirikiana na wamiliki wa vyombo vya usafiri  pamoja na mamlaka tutaweza kudhibiti ajali zisizokuwa za lazima zinazopoteza nguvukazi ya taifa," anasema Bw Kilima.

Anasema, wamiliki wa vyombo vya usafiri wanatatakiwa kuwakabidhi watu wenye stahiki katika vyombo vyao ili kudhibiti tatizo la ajali baharini.

"Hili nalo tumaeliangalia, kwa kiasi kikubwa ndiyo maana tumeamua kushirikiana na shirika la usafirishaji duniani ili kuondoa dosari zilizopo baharini," anasema.

Bw. Kilima anasema kuwa, warsha hiyo itakuwa endelevu ili kuileta hamasa katika kubadilishana ujuzi na uzoefu wa kudhibiti ajali zisizo za lazima baharini.

Zimekuwa zikisaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali za baharini kutokana na wadau kutoka sehemu mbalimbali za usafirishaji kutoa michango yao ya mawazo ni nini kifanyike ili kuondoa tatizo la ajali za baharini.

Anasema kuwa, mwamko wa watu katika taaluma ya ubaharia majini ni mdogo ndiyo maana kumekuwepo na watu wanaoifanya pasipokuwa na sifa stahiki za fani hiyo.

Anasema, hilo ni tatizo kubwa nchini ndiyo maana kumekuwepo na za baharini mara kwa mara.

Hata hivyo anasema kuwa,  ili kuondoa tatizo hilo kunatakiwa kuwepo na wataalamu wenye sifa stahiki katika fani ili kuondoa ajali zisizokuwa na lazima.

"Ajali kama hizi zinaepukika kama kila mwajiri na mmiliki wa vyombo hivi wataamua kuwajiri watu wenye sifa stahiki za taaluma hii," .

Anatoa wito kwa, vijana kusomea taaluma hiyo ili iwe changamoto kwao katika kuhakikisha wanadhibiti ajali za baharini.

Pia, Desemba 7 ya kila mwaka Tanzania na mataifa 190 duniani ambayo ni wanachama wa Shirika la Kimataifa  la Usafiri wa Anga (ICAO) huungana katika kuadhimisha uwekwaji saini wa mapatano ya kimataifa kuhusu usafiri wa anga ulimwenguni.

Maadhimisho hayo pia yamelenga kuwaongezea ufahamu wananchi wa Tanzania juu ya umuhimu wa sekta ya usafiri wa anga katika kuchochea maendeleo ya jamii, kuimarisha uchumi wa taifa na kuboresha mahusiano kati yao na mataifa mengine.

Wananchi hupata fursa kuelezea shughuli na majukumu waliopewa kisheria katika kusimamia na kuratibu usalama na ufanisi wa usafiri wa anga nchini.

No comments:

Post a Comment