23 September 2013

SIMANZI

  • WALIOUWAWA NA AL-SHABAAB KENYA WAFIKA 60
  • MWANADIPLOMASIA WA CANADA NAYE AUWAWA
  • MAKOMANDOO ISRAEL WATUA NAIROBI KUWASAKA
Mmoja wa majeruhi (kushoto) akiwa na jeraha la risasi mgongoni akikimbia kuondoka eneo la tukio.
Watu wakikimbia kuokoa maisha yao baada ya wavamizi kuanza kumiminia watu risasi.

Majeruhi akiwa amebebwa kuondolewa eneo la tukio baada ya kushambuliwa na risasi.
Na Goodluck Hongo

 Idadi ya watu waliokufa katika shambulio lililofanyika katika jengo la kibiashara la Westgate jijini Nairobi nchini Kenya imefikia zaidi ya watu 60 na wengine 162 kujeruhiwa baada ya kundi la watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa kundi la Al-Shabaab kuvamia na kuwamiminia risasi ovyo.


Kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha The Citizen cha nchini Kenya, kundi hilo lilivamia jengo hilo saa saba kasoro dakika 10 mchana juzi na kuanza kuwapiga risasi watu hao. Vikosi vya usalama vya nchi hiyo vikitumia mbwa na helikopta, vimeendelea kuzingira jengo hilo ambapo hadi jana mchana kundi hilo la watekaji lilikuwa bado linawashikilia watu ndani ya jengo hilo la ghorofa nne.

Jengo hilo ambalo ni lenye maduka na migahawa mingi hutumiwa na watu wengi ambapo mara nyingi siku kama ya Jumamosi hujumuika na familia zao kufanya manunuzi ya bidhaa mbalimbali.

Televisheni hiyo ilionesha jinsi vikosi vya usalama vya nchi hiyo vilivyokuwa vikiokoa watu ambao walikuwa ndani ya jengo, huku helikopta za kijeshi zikizunguka jengo hiloTelevisheni hiyo ilisema wanamgambo hao ambao idadi yao haijafahamika bado wamejificha ndani ya jengo hilo wakiwa wamewateka idadi ya watu wasiojulikana wakati juhudi za kuwaokoa zikiendelea.

Mitandao ya kijamii

Katika baadhi ya mitandao ya kijamii ilimnukuu Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, akielezea shambulizi hilo kuwa ni la kigaidi na kwamba kitendo hicho kamwe hakikubaliki.Alisema waliohusika watakumbana na mkono wa sheria. 
Aliongeza kuwa Wakenya hawatagawanyika kutokana na shambulizi hilo na jeshi lake litaendelea kukabiliana na magaidi wa nje na ndani ya taifa hilo. Rais Kenyatta alisema baadhi ya waliofariki ni jamaa zake na miongoni mwa waliofariki ni mwanadiplomasia wa Canada na raia wawili wa Ufaransa.

Taarifa kutoka Ikulu ya Rais wa Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja aliyekamatwa alifariki kutokana na majeraha yake.

Mashuhuda

   Walioshuhudia shambulizi hilo wanasema kuwa waliwaona watu waliokuwa wamejifunika nyuso zao wakianza kumshambulia kila mtu waliyekutana naye ndani ya jengo hilo.Inadaiwa kwamba walikuwa wakiuliza waliyekutana naye maswali na aliyeshindwa kujibu alipigwa risasi.

Uingereza yatoa tamko

   Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, William Hague, alisema Serikali yake inashirikiana na Kenya kuhakikisha magaidi na wanamgambo hao wanapatikana.Hili ndilo shambulizi baya zaidi kuwahi kuikumba Kenya tangu shambulizi la bomu lililotokea mwaka 1998 lililotekelezwa na Al-Qaeda.

   Vikosi vya usalama vikishirikiana na vikosi maalumu kutoka jeshi la nchi hiyo wameendelea kuweka ulinzi mkali ili kuwaokoa watu walioshikwa mateka na watekaji hao wenye silaha nzito kwa majibu wa mashuhuda.

   Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), lilimnukuu Waziri wa Usalama Joseph Ole Lenku, akisema watu 59 wamefariki katika shambulizi hilo lililofanywa na wanamgambo wa Al-Shabaab na wengine 175 kujeruhiwa.Waziri Ole Lenku alisema kuwa idadi ya magaidi walio ndani ya jengo hilo ni kati ya 10 na haijulikani wamejificha sehemu gani katika jumba hilo la Westgate.

Red Cross wanena

   Shirika la Msalaba Mwekundu la nchini Kenya awali katika taarifa yake, lilisema kuwa watu 43 ndiyo waliofariki na zaidi ya 50 kujeruhiwa huku wengine wakitekwa katika shambulizi hilo.
 Habari zinaeleza kuwa hadi jana jeshi limeweza kudhibiti hali nje na ndani ya jengo hilo, magari ya kijeshi yamepelekwa katika eneo hilo, huku polisi na wanajeshi wakijaribu kuokoa mateka.

   Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa na vyombo vya usalama vya nchi hiyo, zinasema wanamgambo hao wako ndani ya duka moja kubwa katika jengo hilo.

Al-Shabaab watamba kuhusika

    Kwa mujibu wa BBC, ofisa mmoja mkuu wa kundi la kigaidi la Al-Shabaab, aliliambia shirika hilo kuwa kundi hilo ndilo limehusika na shambulio hilo.Kwa mujibu wa ofisa huyo mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Kenya kwa kujihusisha na vita ndani ya Somalia ambako wanajeshi wake wanakabiliana na kundi hilo.

  Wanamgambo wa Al Shabaab kupitia kwa mtandao wao wa Twitter , wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.

  Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al-Shabaab limesema kuwa Kenya haikusikia onyo hilo na kuendelea kuwaua Waislamu wasio na hatia nchini Somalia.

  Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwa Shambulio la Westgate ni tone tu katika bahari ya mfano wa yanayowakumba Wasomali nchini Somalia.

Makomando wa Israel wajitosa

  Katika hatua nyingine makomandoo wa Israel jana waliwazidi nguvu wanamgambo wa Somalia na kufanikiwa kuwakomboa mateka waliokuwa wakishikiliwa na manamgambo hao.Milio ya risasi ya hapa na pale ilisikika huku maofisa usalama wa Kenya wakisema walikuwa wakijaribu kuwaua au kuwateka washambuliaji waliobakia na kumaliza umwagaji damu uliodumu kwa saa 28 katika ukumbi wa soko wa Westgate.

  “Makomandoo wa Israel wamekwisha wasili na sasa w a n a w a o k o a ma t e k a n a waliojeruhiwa,” chanzo cha habari cha usalama cha Kenya kiliiambia Shirika la Habari la Ufaransa- AFP. Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel ilikataa kuthibitisha au kukanusha kwamba vikosi vyake vilihusishwa  

2 comments:

  1. Replies
    1. Am very sorry what happen in Kenya since large number of people lost life due to terrorists.let us pray for them so that our God could rest them in peaceful way.others should remain in tolerant spirit during this hardship and difficult period.Amen.

      Delete