Na Rehema Mohamed
ALIYEKUWA Polisi wa
Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Ukonga, G 5226 PC Ramadhani Selemani (27),
amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu kazi Kisutu akikabiliwa na
shtaka la kukutwa na meno ya tembo yenye thamani ya zaidi ya sh.milioni 120.Mshtakiwa mwingine
katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi ni mkazi wa Mbagala Zakhem, Hamis Mwanya
(22).
Mbele ya Hakimu
Nyigulila Mwaseba, ilidaiwa na Wakili wa Serikali Mwanaisha Komba, kuwa
mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo
Julai 19, mwaka huu Tazara Wilaya ya Temeke.Ilidaiwa kuwa
mshtakiwa huyo alikutwa na meno manne ya tembo pamoja na vipande 12 vya meno
hayo mali
ya serikali. Mshtakiwa huyo hakutakiwa kujibu kosa hilo.Upande wa
mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa shauri hilo
bado haujakamilika na kwamba shauri hilo
litatajwa tena Agosti 7, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment