07 September 2012

TFF, Vodacom kufunga 'ndoa' Jumanne ijayo



Na Elizabeth Mayemba

KAMPUNI ya simu za mikononi ya Vodacom inatarajia kuingia mkataba wa Ligi Kuu Tanzania Bara na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jumanne ijayo.


Akizungumza Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa TFF Boniface Wambura alisema wadhamini  hao wataingia mkataba huyo Jumanne katika ofisi zao zilizopo Dar es Salaam.

" Taarifa  rasmi juu ya muda wa kusaini na pande zitakazoshuhudia hafla hiyo itatolewa hivi karibuni, hivyo tutawatangazieni waandishi wa habarim," alisema Wambura

Alisema Ligi Kuu inatarajiwa kuanza kutimua vumbi  Septemba 15, mwaka huu  huku ligi hiyo ikishirikisha timu 14.

Mechi ambazo zitafungua dimba la michuano hiyo ni kati ya  Simba na African Lyon ambao watacheza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Polisi Morogoro na Mtibwa Sugar (Jamhuri, Morogoro), Tanzania Prisons dhidi ya  Yanga (Sokoine, Mbeya), Mgambo JKT  watacheza na Coastal Union (Mkwakwani, Tanga) na  JKT Ruvu wao watacheza na ndugu zao Ruvu Shooting (Azam, Dar es Salaam).

Mechi nyingine ni kati ya  Kagera Sugar  na  Azam (Kaitaba, Bukoba), ambapo Toto African watapambana na maafande  Oljoro JKT  Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Kama ilivyokawaida misimu yote mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Simba na Azam FC inatarajiwa kuchezwa Septemba 11, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa,Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment