20 January 2012

Kuna tatizo la viongozi wasiowajibika

Na Peter Mwenda

SERIKALI inajitahidi kuondolea wananchi wake kero mbalimbali katika sekta mbalimbaliikiwemo Afya, Elimu, Kilimo na Miundombinu.

Lakini watendaji wanaopewa majukumu ya kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo wamekuwa kikwazo hivyo kusababisha wananchi kulalamikia serikali yao kuwa haiwajali.
MBunge wa Jimbo la Kisarawe Bw. Selemani Jafo amekuwa akisimama kidete kushirikiana na wananchi wake kugomea miradi ambayo haijakamilika kulingana na mikataba ilivyofikiwa.
Bw. Jafo ambaye alichaguliwa kuwa mbunge katika Uchanguzi Mkuu Mwaka 2010 (CCM) anasema, udhibiti huo wa miradi ya maendeleo umefanikiwa kwa kiasi lakini bado kuna tatizo kubwa la uongozi usiowajibika katika vijiji vingi vya wilaya ya Kisarawe.
'Kuna watendaji katika sekta mbalimbali katika wilaya hii hawafanyi kazi bila kusukumwa, suala hili nitapambana nalo kuhakikisha kila mtumishi anawajibika, imefika wakati wanakisarawe wenyewe waungane kujenga wilaya yao" anasema Bw. Jafo.
Sekta ya maji
Mbunge Jafo anasema, wananchi wa Kisarawe ambayo wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji wameamua kupunguza matatizo ya maji kwa kuipokea miradi ya kuchimba visima na kusimamia kwa dhati.
Anasema, mradi wa kuchimba visima katika Wilaya ya Kisarawe ilikuwa inanze kutoka Oktoba mwaka jana kwa ufadhili wa mradi kutoka Benki ya Dunia ambako kimechimbwa kisima kirefu katika Kata ya Chole.
Awali anasema, kata hiyo dumu la maji lilikuwa likiuzwa sh. 1,500 kisimani kabla ya kubeba kupeleka nyumbani na maji hayo yalikuwa yakipatikana katika Kata ya Vikumburu ambako wananchi walitembea umali mrefu kuyafuata maji hayo.
Anasema, mpaka sasa vinachimbwa visima katika Kata za Msanga, Vikumburu, Kwala, Chole na Kihale ambavyo vikikamilika na kutoa maji ya kutosha Wilaya ya Kisarawe kwa asilimia 40 itakuwa imepunguza kero ya maji.
Bw. Jafo anasema, kisima cha Boga kilichopo Kata ya Maneromango ni moja ya mikakati ya vijiji vinne ambavyo vitachimbwa visima kwa ajili ya kusambaza katika vijiji vingine.
Kijiji cha Boga ni mfano wa kuigwa na wanakisarawe wengine kwa sababu wako mstari wa mbele kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi.
"Nashukuru kusikia mliwawagomea wachimba kisima ambao walikiuka makubaliano ya kuchimba mita 150 badala yake walichimba mita 100 tu mkiwambia hicho si kisima chenu'alisema Bw. Jafo.

No comments:

Post a Comment