30 November 2010

NMB Iringa kujenga jengo jipya .

Na Eliasa Ally, Iringa

ZAIDI ya sh. milioni  60 zitatumika kujenga Tawi Benki ya NMB katika eneo la Gangilonga  katika Manispaa ya Iringa.Akizungumza ofisini Majira Meneja wa Benki ya NMB Tawi la
Mkwawa Mkoa wa  Iringa  Bw. Atupele Mwakibete alisema kuwa lengo la ujenzi huo ni kuihamisha benki ya sasa ambayo itabomolewa na kujenga jengo la kisasa zaidi katika eneo hilo.


Bw Mwakibete alisema kuwa ujenzi  wa benki hiyo utachukua miezi sita hadi kukamilika  Alisema kuwa mkoa wa Iringa sasa umekuwa na kuzaa mkoa mwingine wa Njombe hivyo na NMB inatakiwa kupanua wigo wa huduma zake.


Bw.  Mwakibete alisema kuwa benki hiyo inatarajia kujenga klabu kubwa ya wateja wa wake ambayo itakuwa na kazi yake  kutoa ushauri kwa benki hiyo ili itoe
huduma bora zaidi kwa wateja wake  kufuta  kero zinazowakabili.

"Tumejipanga na nitahakikisha ujenzi wa benki hiyo mpya unakamilika na uanzishwaji wa klabu hiyo kubwa ya NMB ya Mkoa wa Iringa inakamilika na nitahakikisha kunakuwepo na mafanikio makubwa zaidi na wateja wetu wananufaika zaidi kwa misaada, mikopo pamoja na huduma zingine za kibenki wanazohitaji,"alisema

No comments:

Post a Comment