31 July 2013

MTIHANI WA MAWAKAL FIFA SEPT.26



 Na Ester Maongezi
MTIHANI wa uwakala wa wachezaji na uwakala wa mechi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), unatarajia kufanyika Septemba 26 mwaka huu kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
.Akizungumza Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema katika mtihani huo, kutakuwa na jumla ya maswali 20.Alisema 15 kati ya hayo yanatoka FIFA kuhusiana na kanuni za kimataifa za mpira wa miguu na matano yatatoka TFF, kuhusiana na kanuni mbalimbali zinazotawala mchezo huo nchini.
  Wambura alisema kwa ambao wangependa kufanya mtihani huo, utakaokuwa katika lugha ya Kiingereza ambayo ni moja kati ya lugha nne rasmi za FIFA, wanatakiwa kujisajili TFF kwa ada ya dola 50 za Marekani, ambapo watapewa utaratibu na maeneo ambayo mtihani huo unalenga.“Mtihani huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi na muda wa kufanya mtihani hautazidi dakika 90.“Mpaka sasa Tanzania ina mawakala watano wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA. Mawakala hao ni John Ndumbaro, Mehdi Remtulla, Ally Saleh, Yusuf Bakhresa na Said Tully,” alisema Wambura.

No comments:

Post a Comment