Na Suleiman Mbuguni
KIKOSI cha timu ya Simba, ambacho
kimepiga kambi katika hoteli ya Bamba Beach Kigamboni, Dar es Salaam kujiandaa na Ligi Kuu Tanzania
Bara msimu ujao, kinatarajia kukamilika leo.Akizungumza Dar es Salaam jana Ofisa
Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema wachezaji wao waliokuwa na Taifa
Stars, Amri Kiemba na Haruni Chanongo walitarajia kujiunga jana na kambi hiyo.
Alisema
wachezaji wengine wa kimataifa, Hamis Tambwe wa Vitalo ya Burundi na Gilbert Kazwe nao wanatarajia
kuwasili nchini leo kuungana na wenzao Bamba Beach.“Tunatarajia kwamba kambi ya timu yetu
iliyopo chini ya Kocha Mkuu, Abdallah ‘King’ Kibaden na msaidizi wake, Jamhuri
Kihwelu inatarajia kukamilika leo.
“Na hii ni kutokana na kwamba wachezaji
wetu, Amri Kiemba na Chanongo waliokuwa na Taifa Stars walitarajia kujiunga leo
jioni (jana), huku wachezaji wa kimataifa nao tunawategemea leo,” alisema.
Kiemba na Chanongo walikuwa na Taifa
Stars kwa ajili ya michuano ya kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa
Afrika nchini Afrika Kusini, lakini ilitolewa na Uganda
kwa jumla ya mabao 4-1 baada ya kufungwa bao 1-0 jijini Dar es Salaam na wiki
iliyopita ilifungwa 3-1 Kampala,
Uganda.Kamwaga
alisema wachezaji waliopo kambini wanaendelea vizuri na mazoezi kwa ajili ya
kujiandaa na ligi hiyo na pia katika bonanza lao la Simba Day, ambalo hufanyika
kila mwaka.
No comments:
Post a Comment