01 March 2011

'Safari Nyama Choma' yapamba moto

Na Mwandishi Wetu, Mbeya

MASHINDANO ya 'Safari Lager Nyama Choma 2005', yamepamba moto jijini hapa ambapo tayari bar tano bora zimeshapatikana.Fainali ya mashindano
hayo ya mkoa yanatarajia kufanyika Jumamosi, ambapo majaji kutoka Dar es Salaam wanatarajia kuwasili leo kwa ajili ya kazi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana Meneja wa bia ya Safari, Fimbo Butallah alisema maandalizi ya fainali hizo tayari yamekamilika.

Alizitaja bar zilizopenya hatua kuwa ni Kalembo, 2000 Grocery, Mbeya Carnival Sky Club na Neabana bar.

"Kila kitu kinakwenda vyema kinachosubiriwa ni muda ufike ili mshindi aweze kupatikana na pia tunatarajia kutakuwa na burudani kemkem ikiwemo bendi TOT Plus na Marimba," alisema Butallah.

No comments:

Post a Comment