22 August 2013

NSAJIGWA MWASIKA WAIKWAZA YANGA



Na Amina Athumani
UONGOZI wa Yanga umesema kitendo cha wachezaji wao wa zamani, Shadrack Nsajigwa na Stephano Mwasika kupeleka barua ya madai Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) si cha kiungwana ni cha kuifedhehesha klabu hiyo
.Wachezaji hao waliachwa na Yanga, mara baada ya kumaliza mikataba yao mwaka jana, lakini wanaidai Yanga sh.milioni 16.Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema Yanga haina nia mbaya ya kutaka kuwadhulumu wachezaji hao kwani wamekuwa wakifanya mawasiliano nao ili wawalipe fedha zao.
Alisema kati ya sh.milioni 16 wanazodai wachezaji hao, Nsajigwa anadai sh.milioni 10 na Mwasika sh.milioni 6."Wiki mbili zilizopita tuliwapigia simu wachezaji hawa, ili tujue jinsi gani tutaweza kuwalipa fedha zao, lakini hatukuwapata sasa wanataka kuharibu usajili wetu, sisi hatuna nia mbaya na wachezaji wetu na sidhani kama TFF, watasitisha usajili wetu kwa sababu hiyo," alisema Mwalusako.
Alisema Yanga imepata taarifa za wachezaji hao kupeleka barua za madai TFF, hivyo wameamua kutoa taarifa hiyo kutokana na kwamba huenda shirikisho hilo linaweza kutoa uamuzi utakaoiathiri klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment