JESHI la Zimamoto nchini linafanya
maandalizi ya ujenzi wa vituo vya Zimamoto vya kikanda katika Jiji la Dar es
Salaam ili kusogeza huduma kwa wananchi, anaripoti Charles Lucas.
Akizungumza
wakati wa hafla ya kuwapandisha vyeo baadhi ya maofisa wa jeshi hilo, Dar es
Salaam jana Naibu Kamishna Jenerali wa jeshi hilo, Luteni Kanali Saimon Mgumba
alisema ili kuboresha huduma kwa wananchi watajenga vituo visivyopungua vitano
jijini.
Kamishna huyo
alisema, kwa kuanzia utekelezaji wa mpango huo maeneo yaliyopangwa kujengwa ni
Mbagala, Lugalo, Gongolamboto, Mwenge, Kigamboni na Mabibo na siku zijazo vituo
vitajengwa katika maeneo mengi zaidi.
Pia aliwaomba
wananchi ushirikiano yanapotokea majanga ya moto ili kazi ya kuudhibiti kuwa
rahisi na kuonya baadhi ya watu wenye tabia ya kupiga simu katika jeshi hilo na
kutoa lugha za matusi na kejeli kuwa kuanzia sasa watachukuliwa hatua za
kisheria.
“Tumekuwa na
wakati mgumu katika utendaji tunapigiwa simu zaidi ya matukio 20 ‘hewa’ ni
hasara kwa taifa tunatumia fedha kufika maeneo ambayo hakuna tukio, hivyo
tumefunga mitambo ya kutambua watu wanaofanya mchezo huo mchafu,” alisema.
Upandishaji wa vyeo kwa maofisa hao wanaotoka
mikoa mbalimbali ni mwendelezo wa maboresho ya jeshi hilo linalojetegemea
katika utendaji wake zaidi ya maofisa 500 wamepandishwa vyeo hivi karibun
No comments:
Post a Comment