30 July 2013

TRA YAANZA MFUMO MPYA ULIPAJI KODI MAGARI



 Na Fatuma Mshamu
MAMLAK Ay aMapatoTanza ni a(TRA ),im et angazakua nzakw amfumompyawaulipajiwa adaz amagari kwa mwakakwanjiaya mt andaoutakaoa nzakutumika Agosti Mosi mwakahuu .Hayoyame ele zwajanajijini Dar es S alaamnaMku rugen zi waHudumana Elimu kw aMlipakodi Richard Kayomboa lipokuwaaki elezamabor eshoy amfumowakielek tronikiamba om amlaka hiyo inaendelea kufanya ikiwa ni juhudi za kuboresha huduma kwa walipakodi.

Alisema mfumo huo utatumika kulipa ada za mwaka za magari ambapo mlipakodi anaweza kupata taarifa ya kiasi cha kodi anachotakiwa kulipa. “Mfumo huu ni rahisi kutumia na utapunguza misongamano isiyo ya lazima katika mamlaka ya mapato na mabenki na hivyo kumwezesha mlipakodi kulipa ada ya gari lake akiwa mahali popote nchini pia mfumo huu unapanua wigo wa njia za kulipa kodi na mlipaji yuko huru kuchagua njia aipendayo”, alisema kayombo.
  Alisema malipo haya yanaweza kufanyika kwa njia ya M-pesa, Tigopesa, Airtel Money na kwa wakala wa Maxmalipo ambapo hurahisisha kazi katika ofisi yoyote ya TRA kwa kupewa stika ya kuonyesha namba ya kumbukumbu iliyotumika kufanya malipo.
“Ili kuweza kuchukua kadi ya gari, mlipa kodi anatakiwa kuwa na leseni ya udereva au hati ya kusafiria, pia mfumo huu ni muendelezo wa maboresho ya mfumo wa kulipa kodi kwa mtandao (revenue gateway) uliobuniwa na TRA kwa kushirikiana na Benki Kuu (BoT),” alisema Kayombo.Aliongeza kuwa, wananchi wote wanaolipa ada za magari huitumia fursa hiyo ya kulipa kodi kwa njia ya mtandao ili waweze kuendelea vema na shughuli za ujenzi wa Taifa badala ya kutumia muda mwingi katika misururu kwenye mabenki.

1 comment:

  1. Sasa wale "vishoka" wa pale TRA - Moshi wataishije? Na wale wafanyakazi wa TRA - Moshi waliowajiri "vishoka" hao nao wataponea wapi? Au wataishia kubuni mbinu nyingine nini!! Hebu tusubiri; yetu macho kwani mvunja nchi ni mwananchi!!!!!

    ReplyDelete